Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi nichangie bajeti hii ya kihistoria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Comrade Senator Ndassa amesema kwa uzoefu wake wote aliokaa katika Bunge hili, hajawahi kuiona bajeti iliyoshiba na yenye matumaini kama hii. Na mimi pamoja na umri wangu huu mdogo, toka nimeanza kupata ule ufahamu kuweza kujua redio, tv na kuweza kusoma na kuandika sijawahi kuiona bajeti iliyosheheni matumaini kama hii. Bajeti hii ni bajeti ya wananchi, bajeti hii inawagusa wakulima wote, wafugaji, wafanyabiashara wa kada zote na bajeti hii inawagusa wawekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba bajeti hii ni bajeti ya pili ya Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imejipambanua kwamba inakwenda kuitengeneza Tanzania ya viwanda na kumuondoa Mtanzania angalau ifikapo mwaka 2025 tufike katika level ya kati ya uchumi. Kwa namna yoyote ukitizama bajeti hii, imefanikiwa kutujibu swali la siku zote la tafsiri ya maendeleo, maendeleo ni nini? Bajeti hii imetujibu development should be people centered. Kwa namna yoyote utakapoingalia inakuonyesha bajeti hii ni bajeti ya watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi bajeti hii imejikita katika kuwasaidia watu wa uchumi wa chini, uchumi wa kati, wafugaji, wakulima, wafanyabiashara na wawekezaji. Ili twende vizuri na tuelewane katika hili kuwaambia kwamba bajeti hii ni bajeti ya kihistoria, naomba niwapeleke kwenye mambo kumi muhimu yaliyopo kwenye bajeti hii. Kwa lugha nyingine naweza kuyaita ten tenants. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Taifa lolote unaweza kulipima kama lina matumaini kuhusu kesho baada ya miaka kumi na miaka 50 ijayo kwa namna gani inajikita kwenye miradi mizito ya vielelezo, miradi ya maendeleo. Bajeti hii imeanza pasipokuwa na shaka lolote kutekeleza miradi ya vielelezo zaidi ya saba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa kwanza ni ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge. Ni watu tu ambao hawafikiri dunia inakwendaje wanaweza wakahoji hili. Kwa miaka yote tumelalamika kwamba reli ya kati kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma kwamba bidhaa zinakwenda shida, maendeleo hayawezekaniki, tumetoka sasa tunakwenda kwenye standard gauge. Dola bilioni 300 zimekwishatengwa na tayari zimekwenda kwenye kuandaa karakana na kufanya upembuzi yakinifu ili ndani ya hii miaka michache, mtu anatoka Dar es Salaam mpaka anafika Kigoma akiwa amelala usingizi, anasoma gazeti lake kwa muda wa saa saba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuboreshwa kwa Shirika la Ndege Tanzania. Hili kuna watu hawalielewi, wakiambiwa Serikali imenunua ndege huwa haelewi. Unaponunua ndege hatuangalii mapato yanayopatikana kwa wewe kupanda ndege kutoa hapa kwenda Kigoma, Songea na sehemu nyingine. Tunaangalia vitu vingine vinavyosababisha kukua kwa uchumi lakini kwa sababu umetumia saa chache sana barabarani, uchumi unakua. Hii ni hatua kubwa sana ya nchi yoyote inayotaka kwenda kwenye uchumi wa kati lazima iimarishe shirika lake la ndege. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa tatu, tumezungumzia sana suala la Mchuchuma na Liganga, hii imewekwa katika mpango huu. Tushukuru sana Serikali tumeipigia kelele sasa tunakwenda ile hoja mliyokuwa mnalalamika chuma sasa kinatoka Liganga na makaa ya mawe yatatoka Liganga. Utaratibu wa reli sasa haitakuwa ya kati tu, kwa chuma cha Liganga tunao uwezo wa kuuza chuma nje, tunao uwezo wa kutandaza reli kwenye Wilaya zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa nne ni ununuzi na ukarabati wa meli kwenye maziwa makuu. Juzi tulipokuwa tunaongelea hapa Wizara ya Uvuvi, ndugu yangu Ulega alisema hatutumii vizuri ile bahari kuu kwa sababu hatuna meli za kisasa zenye uwezo wa kuvua, sasa Serikali imeiona hili na imeliweka. Sasa nashangaa watu wanaosema hawaoni basi yawezekana ni vipofu tuwasaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tano ni ule wa gesi kimiminika (liquefied natural gas). Hili ni jambo kubwa ambalo sasa litakwenda kujibu matatizo mengi. Ile gesi ikishafika tunaiboresha sasa itakaa kwenye mitungi ni hatua ya baadae hata yule aliyekuwa anatia mashaka mafuta ya taa yamepanda bei, huko sisi tunataka kutoka, mafuta ya taa kwanza yanaleta air pollution, ni adha na ukipika na chakula nacho kinanuka, tunataka tumtoe mtu huyo huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mama yangu ulinifundisha siwezi kukusema sana ila ili kuweka tu kumbukumbu sahihi, siyo sawa unaposema kuhusu mafuta ya taa. Hesabu zote za kiuchumi zinatuonyesha tunatoka kwenye mafuta ya taa tunakwenda kwenye gesi. Mwalimu wangu wataalam wanasema you can not strengthen the weak by weakening the strong. Hoja ya msingi ni kumfanya yule weak awe strong siyo kwa kumdhoofisha yule ambaye ni strong. Kupeleka bei ya mafuta kwa wale watu wenye magari hakumaanishi kuwa tunamfanya huyu asiyekuwa na uwezo awe weak, tunajaribu kumuimarisha kwa njia nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili katika mambo yangu yale kumi, hili lilikuwa la kwanza tu, la pili ni Kodi ya Majengo. Sheria ya Fedha ya mwaka 2016 ndiyo kwa mara ya kwanza iliyoipa mamlaka TRA kukusanya mapato kwenye majengo. Safari hii imefanya maboresho tu kwa sababu ilikuwa haieleweki watu wanakadiriwa vipi, Serikali imekuja sasa na ukomo, nyumba ya kawaida iwe shilingi 10,000, ya ghorofa shilingi 50,000, tatizo liko wapi hapa sasa? Unaona sasa tunataka tupate mapato katika njia inayoeleweka, kila nyumba itatoa Sh.10,000 kila ghorofa shilingi 50,000, Serikali inayotabirika katika maendeleo ndiyo inakuonyesha namna gani itatutoa hapa tulipo itupeleke sehemu nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wafugaji, Serikali imeondoa VAT kwenye mayai ya kutotolesha vifaranga (fertilized eggs for incubation), jambo hili ni kubwa sana.

Ndugu yangu Mwita pale atakuwa shahidi kule Kitunda, walishaacha sasa kuleta mayai pale mjini kwa sababu gharama za chakula na kutotolesha vifaranga ilikuwa kubwa kutokana na kodi hii. Kwa kuiondoa kodi hii sasa unamsaidia mtu wa kawaida wa chini, wale vijana na akina mama watakuwa wanafuga kuku na kutotolesha mayai. Hapa sasa ndiyo hatua ya kwanza ya kutengeneza viwanda vidogo vidogo vya kusindika nyama na ku-process mayai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni viwanda na uwekezaji. Serikali imeondoa VAT kwa uagizaji wa bidhaa za mitaji yaani capital goods, hili jambo linasaidia kwanza kuwa-encourage Watanzania wawe export oriented. Huwezi ukapata pesa za kigeni kama hau-export lakini vilevile tukumbuke Tanzania it’s a strategic area, tuna-control hizi land locked countries, tukiwa na mfumo mzuri wa kuondoa hizi kodi na kupeleka malighafi nje…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.