Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sandiangu wa ukulu kabisa, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia hoja hii iliyo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kuunga mkono hoja hii mia kwa mia. Nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Makatibu Wakuu na wataalam wote waliotayarisha Bajeti ya mwaka huu. Ahsanteni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijachangia, kuna jambo moja dogo linanikera sana, naomba niliseme hapa hewani. Terehe 2 Juni, kwenye Bajeti ya Wizara ya Nishati, Mheshimiwa Saed Kubenea alisimama hapa akinituhumu mimi Mwambalaswa kwamba kwanza ni Mkurugenzi kwenye Kampuni ya Umeme ya Upepo ya Singida na kwamba Ukurugenzi wangu huu nina mgongano wa maslahi (conflict of interest) kwa sababu nilikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na vilevile nilikuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCO. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna project nyingine ya umeme wa upepo, kule kuna concept, kuna idea na idea hii imeanza mwaka 2000. Mimi nimekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati mwaka 2013, hii imeanza mwaka 2000. Mgongano wa maslahi unatoka wapi? Nimekuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCO mwaka 2008. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kubenea alienda mbali zaidi, akasema Mheshimiwa Mwambalaswa alizuia kutekeleza Ripoti ya Richmond ya Mheshimiwa Mwakyembe. Mimi Mbunge nitazuiaje ripoti? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huyu Mheshimiwa ananisemea maneno ya uwongo bila sababu yoyote. Ananishambulia bila sababu! Kule kuna concept, is not a company! Is not a project, is a concept. Ni ya waswahili fulani, sisi na walimu wa Chuo Kikuu tumeacha wazo hilo, lakini linapigwa vita na watu kama yeye. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani yeye Mheshimiwa angeona hii concept ni ya mzungu angeunga mkono kama vile ambavyo Mheshimiwa Rais amezuia makontena ya makinikia, amempinga, lakini angezuia mzungu, angemuunga mkono. Jamani tusitembee na Ph.D mifukoni za mitaani. Ph.D (Pull him Down). Tuinuane waswahili kwa waswahili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kubenea namfahamu sana, ni mdogo wangu, rafiki yangu wa miaka mingi. Alipoanzisha Kampuni ya Jarida lake la Mwanahalisi, mimi na wenzangu tulimchangia computer yake ya kwanza tulinunua sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulimnunulia, lakini unaona anakonipeleka! Mheshimiwa Kubenea alimwagiwa tindikali machoni; amelazwa hospitali, Mheshimiwa Rais Kikwete, Rais wa Awamu ya Nne ameenda kumwona hospitali na amemchangia pamoja na sisi aende akatibiwe India, akageuka na magazeti yake anamshambulia Mheshimiwa Kikwete. Huyo! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya, Mheshimiwa Kubenea amechukua miaka kama nane anamshambulia Mheshimiwa Lowassa kila siku, ona! Lowassa katika kashfa mpya, hilo hapo; Rostam Hajaandika, hilo hapo; Wanaomsafisha Lowassa Hawa Hapa, hii hapa; Genge Laundwa Kumkabili JK, hili hapa; Rostam Aziz Hashikiki, hili hapa; Mabilioni Yatengwa Kumsafisha Lowassa, hili hapa; Lowassa Kutinga Kortini, hili hapa; kila siku! Leo anamsujudia Mheshimiwa Lowassa, huyo huyo! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi lile ni wazo, sina con- flict of interest yoyote, ni wazo. Kama ana matatizo na mimi aje tuongee. Mimi ni rafiki yangu, namfahamu huyu kijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hilo, nasema hivi, sijui kama anatumwa na dhamira yake au analipwa. Sijui.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuwapongeza Wataalam na Mheshimiwa Waziri kuhusu bajeti iliyo mbele yetu, bajeti nzuri sana, mti wowote wenye matunda unapigwa mawe. Kwa hiyo, mawe tunayategemea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahi sana kwamba barabara yangu ya Mbeya - Chunya - Makongolosi imefika Chunya kilometa 72, ahsante sana Serikali ya JK na Serikali ya Mheshimiwa Magufuli ahsanteni sana. Nimefurahi kwamba kwenye bajeti hii ambayo iko mbele yetu, sasa wanaanza kujenga Chunya kwenda Makongolosi na Mkola na wanafanya kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais kwenye kampeni kwamba tuanze Makongolosi kuja Chunya. Wataalam wako pale kwenye manunuzi, ninashukuru sana na nimefurahi sana. Najua huku kutoka Mkiwa kwenda Itigi iko kwenye bajeti, itaanza kujengwa ili baadaye tukutane katikati hii barabara ambayo zamani ilikuwa the Great North Road iwe kwa kiwango cha lami barabara nzima. Nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, reli ya TAZARA, kama ilivyo reli ya kati ambayo sasa inaboreshwa na Serikali hii ili tutumie uchumi wetu wa jiografia, tutumie nchi yetu kijigrafia kuweza kuzihudumia nchi ambazo ziko landlocked, ili tuweze kuinua kipato na uchumi wa nchi yetu; na reli ya TAZARA iko hivyo hivyo. Reli ya TAZARA yenyewe iko zaidi ya meter gauge, ndiyo maana matreni ya Afrika Kusini yanaweza kupita kwenye reli hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, haihitaji maboresho ya makubwa sana, inahitaji tu labda kuweka umeme ili treni za umeme zipite. Ile ya Kati inapokuwa imekamilika na ya TAZARA nayo iwe imekamilika tuweze kuihudumia Zambia, Zimbabwe, Malawi na Kongo ya Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja wa ndege wa Songwe, nashukuru sana Serikali za awamu zote kwa kujenga uwanja wa ndege pale Songwe, Mkoa wa Mbeya. Uwanja ule uko very strategic kwa kutega uchumi kwenye Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini na nchi zote majirani zetu, lakini sasa hivi taa hazipo za kuongoza ndege. Ndiyo maana mara moja, mbili, tatu ndege inakwenda, inakuta ukungu, inarudi Dar es Salaam hasa wakati wa mvua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba bajeti ya mwaka huu hii ambayo iko mbele yetu, najua fedha imo, tukamilishe kuweka taa kwenye uwanja ule ili tuweze kupata fursa zote za kiuchumi kwenye uwanja huo wa Songwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii bajeti ni nzuri mno, siyo ya kuisemea sana, ni ya kuunga mkono moja kwa moja. Naunga mkono hoja.