Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Bismillah Rahman Rahim.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na kabla sijaanza nina maombi, naomba uniongezee dakika kumi ili nitoe somo leo humu Bungeni. Pili, nakusudia kusema ukweli ili tuondoke hapa tulipo twende mbele na ukweli unauma kwa hiyo nakuomba univumilie na Wabunge wa pande zote wanivumilie. Kama umeniruhusu uniambie ili nijue najipanga vipi katika hoja zangu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nawaomba Wabunge kwanza tuache ushabiki wa kufuata ngoma. Naomba mnisikilize vizuri nitakayoyasema. Kama nchi yetu inapita katika kipindi kigumu au ilishawahi kupita, nchi yetu sasa hivi inapita katika kipindi kigumu sana. Vita hii ambayo Rais John Pombe Magufuli anaendelea nayo ni vita moja ngumu sana na yeye peke yake kama yeye hawezi kufaulu katika vita hii ni lazima Watanzania tushirikiane tukiwa kama Watanzania na siyo CCM, Wapinzani au nani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vita hii ni kubwa kwa sababu ni vita ambayo imekamatana na kitu ambacho ni fitna, kitu ambacho ni mali/fedha. Kwa hiyo hii ni vita moja kubwa sana ambayo ni lazima kama Watanzania tukae pamoja, Waheshimiwa ni lazima tuondoe tofauti zetu. Suala la wana CCM kutuona sisi Wapinzani kama maadui au wakoloni tunaotoka nchi nyingine tunataka kuitawala Tanzania halitatufikisha. Suala la sisi Wapinzani kuwaona CCM ni maadui, ni wezi, ni nani, ni nani halitatufikisha lazima tukawe kitu kimoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpasuko uliopo ndani ya nchi yetu hivi sasa kama hatujatumia busara, hekima na akili zetu, wallah wabillahi wataalah na hii Ramadhan, Tanzania ndiyo imefika mwisho wake hapa. Nayasema haya leo, wenye kuweka kumbukumbu waweke. Tulipo ni pabaya sana kuliko

kipindi chochote kile ambacho nchi yetu imepitia. Vita hii ni ngumu na vita hii inahitaji umoja wa kweli kweli. Tufanye nini ili tutoke katika mkwamo huu tuliokwama? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lazima turejeshe umoja wa Kitaifa. Hatuwezi kuondokana na matatizo haya kwenye nchi hii lazima tukae pamoja kama Taifa, tuache kubaguana kwamba huyu Mpinzani, huyu Chama Tawala ana nguvu au ana hiki! Tukae pamoja tuweze kuweka mfumo mmoja wa Kitaifa, tuwe na National vision, tunataka nini kama Taifa ili Rais Magufuli leo vita hii anayoyoiendeleza najiuliza baada ya miaka kumi akiondoka anayekuja ataiendeleza? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama hakuendeleza anayekuja tutakuwa tumefanya nini? Leo anakamatwa Chenge, anakamatwa Ngeleja, anakamatwa mwingine tunawatoa kafara. Mheshimiwa yaliyotokea ni mfumo na lazima Chama cha Mapinduzi kikubali kubeba lawama hii, tufike mahali tusameheane, tufike mahali tukae pamoja, ndiyo kwa sababu Chama cha Mapinduzi ndio kinachoongoza dola. (Makofi)


Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni lazima wakubali kubeba msalaba huu kwamba jamani tumekosea na tulipofika sasa tukae pamoja kama Taifa tuzungumze tuwe na mfumo mmoja wa Kitaifa ambao utatuondoa hapa tulipo kutupeleka mbele. Malumbano haya tunayoendelea nayo hatutafika hata siku moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpasuko huu, hawa wanaotajwa tajwa ni wanadamu, wanadamu, wana nyongo, wana fikra na wana watu nyuma yao, wanaumia, wanavumilia lakini ipo siku watasema, mwisho wa siku Taifa hili tutakuwa tunalipasua sisi wenyewe. Ni wakati sasa tukae pamoja kama Taifa, tuangalie tunataka nini katika kila sekta tuwe na vision tunataka nini.

Mheshimiwa Spika, leo akiwa Mheshimiwa Magufuli ndio Rais aende hapo atupeleke katika vision hiyo, kesho akija

Mlinga ndiyo Rais wa Tanzania atupeleke hapo, sitaki ushabiki nimesema Waheshimiwa, sio kwamba Mlinga amekuja anasema yeye kwa sababu ni mpenzi wa mpunga tunaondoka katika hapa leo tulime mpunga ili tusafirishe nje ya nchi, hapana! (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, tusiwe hivyo tuwe na National Vision ambayo kila Kiongozi anayekuja awe wa Chama Tawala, awe wa Upinzani anatupeleka hapo, tutakuwa tumeondokana na hili, vinginevyo narudia tena Wallah wabillah watallah vita hii hatutashinda na tutagawanyika na kama Taifa hili litatawanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa kuna fitna na mali ni fitna na hili Mwenyezi Mungu amesema hii ni fitna na tusipokuwa makini Taifa hapa ndio linafikia mwisho wake.

Mheshimiwa Spika, niseme hivi, namuunga mkono Mheshimiwa Rais Magufuli, katika vita hii na namuunga mkono kwa sababu ameamua kujitoa muhanga, nilikuwa nafikiri Rais Magufuli yupo katika zile sifa za unafiki lakini hayumo na ndio maana nikasema ni mfumo. Alipotoka kwa sababu kipindi kilichopita alikuwemo katika Baraza la Mawaziri, alikuwemo ndani ya Serikali na haya yote yanayotendeka leo yeye alikuwemo alisema? Alitakiwa aondoe kwa mkono wake wakati ule hathubutu, alitakiwa aseme hathubutu, lakini alichukia, leo amefika mahali anaweza kuondoa kwa mkono wake anaondoa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, waliopo hawa Mawaziri hawa tusidanganyane hakuna mmoja anayeweza kumwambia Rais hili usifanye, hakuna!

Mheshimiwa Spika, mfumo ambao ulijengeka haumwezeshi Waziri yeyote aliyepita au Mwanasheria Mkuu au yoyote kuweza kumwambia Rais usifanye hili hayo ni makosa yametendeka na mwanadamu yeyote lazima afanye makosa ndio akawa binadamu, ambaye hafanyi makosa ni Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo niwaombe, niwaombe ndugu zangu wa CCM mbadilike, mkubali kwamba Taifa hili ni letu sote tukae pamoja tuseme nini vision ya Taifa katika kila idara, katika kila sekta ili tujenge nchi yetu kwa pamoja. Malumbano hayatatusaidia, nguvu zenu za dola hazitasaidia na hapa Taifa litagawanyika na tutagawana mbao kuanzia hapa.

TAARIFA .....

MHE: YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa kwa sababu tatizo lililopo inapoletwa sheria hapa Bungeni, unapoletwa Muswada wowote hapa unakuja

na maagizo, inatakiwa Wabunge waachwe huru, wawe huru kujadili, wawe huru kuishauri Serikali, yasiletwe maagizo kwamba Caucus ya CCM ikutane twendeni hivi, Caucus ya UKAWA ikutane twendeni hivi, tuwe huru kujadili mawazo, kujadili masuala ya Taifa letu, mhimili huu usiingiliwe, Rais abaki na Muhimili wake, atuache Wabunge tuweze kusaidia Taifa hili. Tukienda na tabia hii tutalimaliza Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu ya pili, naenda kwa Mheshimiwa Waziri, nimwombe Mheshimiwa Rais a-pause kidogo huko kwenye madini, kwa sababu huu uchafu na uozo huu upo nchi nzima, katika Wizara zote na Idara yote na Taasisi zote. Baada ya pato ambalo litapatikana huko kwenye madini na sehemu nyingine, upotevu na wizi wa namna hiyo hizo fedha zikipatikana zinaenda wapi? Zitakwenda Hazina, Wizara ya Fedha huko ndio kumeoza ndio kwenye wizi ndio kwenye ubadhirifu mbaya kupita wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Waziri waanze hapa, nataka tuiangalie Benki Kuu kuna matatizo, sitaki kuingia kwenye mambo ya watu sana hapo. Ninachotaka kusema tu, tuiangalie ndoa ya Benki Kuu na Bureau de Changes kuna nini hapa? Pia tuangalie ndoa ya TRA na hawa watu wa clearing and forwarding, kuna upotevu mkubwa wa fedha katika eneo hilo, Mheshimiwa Waziri aangalie tusafishe hapo ili fedha yetu itakapotoka hapo sasa kwenye madini, kwenye uvuvi, kwenye maliasili, kwenye kilimo ikienda pale Hazina tuwe na uhakika fedha yetu ni salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba univumilie nitapiga nikilegeza kidogo mshipa si msumari, lakini tunahitaji kuwa katika umoja huo ili tuondokane na hili tulilonalo. Naiomba Serikali kwa heshima zote, kwa heshima zote tuachane na kubaguana, tuachane na Rais leo kutuona sisi Wapinzani kama maadui, tukae pamoja tuweke mustakabali wa Taifa letu ili tuondoke hapa tulipo twende mbele.

Mheshimiwa Spika, nije kwenye kuchangia na kuielekeza Wizara katika mapato, suala la kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi. Mheshimiwa Waziri amezungumza tu lakini hakueleza na ndio pale niliposema tunahitaji vision, je tunataka kukuza kilimo, lakini ni kilimo gani?