Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nianze kwa kuwashukuru sana wote ambao mliniombea wakati nilipokuwa naumwa. Nashukuru uongozi wa Bunge na Wabunge wote, nawashukuru sana wananchi wa Tarime, nawaambia nimepona. I am back firing.

Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kwa kodi ya majengo (Property Tax). Essence ya kuweka Property Tax mijini ilikuwa ni kuweza kukusanya kodi ili isaidie kusafisha majitaka mijini; kwa ajili ya zimamoto, kwa sababu watu wanaomiliki nyumba, wanalipa kodi ya ardhi na kodi ya pango la ardhi. Sasa Mheshimiwa Waziri amepeleka kodi mpaka vijijini pale ambapo tu ili mradi mtu amejenga nyumba ya tofali na bati ambapo Serikali hawajamnunulia hawajamchangia kwenye tofali, hawajamchangia kwenye cement na vitu vyote hivi alinunua vimelipiwa kodi, wanataka waende kuwachaji watu maskini wa vijijini kodi ya nyumba.

Mheshimiwa Spika, hili ni jambo baya na halikubaliki na ni lazima kwa kweli walingalie, wa-recitify hili, huwezi leo kwenda kuwachaji watu ambao huwapelekei huduma ya zimamoto wala huduma ya majitaka, unakwenda kuwachaji pesa ya kodi ya property tax, unawachaji kwa sababu gani?

Mheshimiwa Spika, la pili, wanaondoa Property Tax kwenye Halmashauri ambapo kama leo wanafuatilia Kenya; jambo ambalo linamtikisa Uhuru Kenyatta na linataka kumtoa madarakani ni mambo mawili tu. Ni kodi, ni kushindwa kugatua pesa kwenye kitu wanachoita County. Wanashindwa kushusha pesa kule chini ili ziende kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa leo wanachukua pesa ambazo kule chini tuna Madiwani, wanalipwa ili wakae vikao, wajadili, wapange huduma kule chini; wanazichukua, wanazileta zote mjini. Leo wanataka watuambie kuwa Serikali hii ina uwezo wa kujadili Kitongoji kimoja kimoja! Kwa mfano, kule Kehero kwetu Kemakorere; wajadili maji kutoka Dar es Salaam yaende kule, haiwezekani. Ndiyo maana tulianzisha Halmashauri ziwe karibu na wananchi zione huduma ndogo ndogo pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, choo kikibomoka kwenye Shule ya Msingi, asubiriwe Mheshimiwa Waziri kwa sababu amechukua Property Tax ndiyo apeleke pesa choo kiende kutengenezwa, watu waende kutumia! Hilo halitawezekana Mheshimiwa Waziri. Hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, ni Road License. Hii ni aibu! Leo wanataka kuwapelekea akinamama vijijini Road License wanaotumia mafuta ya taa kwenye koroboi, yaani maana yake ni kwamba kibatari wanatakiwa kukilipisha Road License, hii itafanyika Tanzania peke yake. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri hili ni muhimu akaliangalia.

Mheshimiwa Spika, la tatu, uporaji wa ardhi Tarime. Kuna kiwanda kimeletwa pale, nami nimesema na mwingine alikurupuka humu, hana research, akaongea wakati nikiwa naumwa.

Mheshimiwa Spika, sipingi kiwanda, lakini napinga utaratibu wa ardhi ya wananchi wa Tarime ambayo ni ndogo sana inavyotaka kuchukuliwa kwa nguvu. Wanakwenda wanaweka beacon kwenye ardhi za watu, mashamba ya watu ambapo Sheria Na. 5 ya mwaka 1999 inasema, ili uchukue ardhi ya mtu, ni lazima umlipe fare prompt and adequate compensation.

Mheshimiwa Spika, hilo halijafanyika, wanatumia nguvu, wanatengeneza makinikia nyingine pale Tarime. Nasi watu wa Tarime mnatufahamu; kwenye ardhi tunailinda kwa nguvu zote. Tutailinda!

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni vyema wakaangalia hilo la ardhi. Juzi wamemwingiza Makamu wa Rais kwenye mkenge kwa makusudi, wanataka kupora ardhi waweke pale kiwanda, mwisho wa siku itakuwa kama hili la makinikia ambalo tumelisema miaka yote, unamchoma mtu kisu halafu unachomoa unamchekea, yaani CCM iliwachoma Watanzania kisu kwenye madini sasa imechomoa kisu halafu inashangilia. Hayo ndiyo yanayotaka kufanyika pale. Kwa hiyo, ni muhimu yakaangaliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la nne, ni suala la madini. Kama kuna watu wameumizwa, kama kuna watu wana vilema, kama kuna watu wana kilio cha madini kwenye nchi hii, ni watu wa Tarime, ambao wamezika ndugu zao miaka na miaka, kwa sababu ya kupigania madini yao yaliyokuwa yanaporwa na sasa wamethibisha yale tuliyoyasema kwamba madini yalikuwa yanaporwa miaka yote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hili nashauri kama Rais yupo serious alete constitution amendment hapa tuwaondolee kinga Rais Mkapa na Rais Kikwete wachunguzwe kwenye suala hili la madini. Baraza la Mawaziri, wanajua wanavyofanya kazi, huwezi kuniambia kwamba Mheshimiwa Daniel Yona aliondoa fifteen percent yetu peke yake bila concert ya Rais.

Mheshimiwa Spika, haiwezekani kama leo Rais anavyonunua Bombadier, haijapitishwa kwenye utaratibu wa kibajeti, haiko popote, uje uniambie kwamba kuna Waziri hapa anaweza kumwambia Rais tusifanye hivi? Au Rais mwingine mwaka unaokuja aje amkamate Mheshimiwa Mbarawa bila Rais kuchunguzwa! Kwa hiyo, tunataka constitution amendment, hawa watu wachunguzwe waonekane nini mkono wao kwenye hili suala? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine, kwa sababu wamedhibitisha kwamba Acacia ni kampuni fake, ni kampuni hewa ambayo haipo na iko Tarime inawaibia wananchi wa Tarime, kuanzia leo nawaambia wananchi wa Tarime wajiandae tuingie mle mgodini tuchukue kila kilicho chetu. Nami hili nalisema humu na nitalifanyia kazi na sidanganyi kwa sababu wananchi wa Tarime wameumizwa na kampuni ile Rais amesema ni fake na hakuna formula ya kukamata mwizi.

Mheshimiwa Spika, mlisema wenyewe na Bunge limesema, formula ya kukamata mwizi ni kupambana naye. Sisi hatutaruhusu madini yatoke pale. Ndege ikitua, itapigwa mawe na hilo linaendelea na organization pale. Magari yao tutayakamata. Kwanza tunawadai fidia nyingi kweli kweli, pale Tarime. Tunataka hayo mambo yafanyike sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, sisi tulitegemea tumwone Rais anaagiza kwamba kuanzia sasa madini yoyote yasiondoke nchini mpaka hayo mambo yote yapitiwe, tutazuia mchanga, dhahabu inaondoka. Hili halieleweki!

TAARIFA .....

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Spika, sipokei. Nami nilijua tangu mwanzo kwamba hamtavumilia tupigane vita hii. Mnafanya mambo ya ukinyonga.

Mheshimiwa Spika, mwizi hana formula. Mheshimiwa Rais amesema Acacia ni mwizi. Yaani wewe unataka tupate utaratibu wa kukamata mwizi Tarime? Sisi watu wetu Mheshimiwa Spika wewe unajua ukiwa Naibu Spika, wameumia na maji ya sumu. Ngombe wamekufa, watu wamepigwa risasi kwa mujibu wa ripoti ya Waziri wa Nishati na Madini; watu wa Tarime zaidi ya 64 wameuawa; na hao ni kwa mujibu wa ripoti ya Mheshimiwa Waziri peke yake. Wameuawa pale mgodini Serikali hii ikilinda wezi wa Acacia. Ndiyo maana nasema watu wengine tuna machungu na tuna maumivu na hili.

Mheshimiwa Spika, mimi nasema na kama mtanikamata, Watanzania watajua hamko tayari kupigana vita hii ya kuokoa rasilimali hizi. Watu wa Tarime wajiandae waanze maandalizi, tuone atakayeenda kulinda mwizi pale, tumwone! Kama Serikali hii itaruhusu Polisi waende kulinda magari ya mwizi.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine kwenye haya ya madini, rasilimali za nchi hii zinazoibiwa siyo madini peke yake, wala siyo Acacia peke yake inayotuibia. Geita Gold Mine inatuibia, magogo ya nchi hii yanasafirishwa nje bure. Twiga walisafirishwa kutoka kwenye nchi yetu hii, wengine wako humu tunawafahamu, waliosafirisha twiga wako humu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu wa Loliondo wanalia mpaka sasa hivi kwa rasilimali zetu zinazoibiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante.