Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema lakini vile vile nichukue nafasi hii kuweza kumshukuru sana Rais wangu Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri sana ambayo ameendelea kuifanya kwa ajili ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijaribu tu kugusia mambo machache katika hotuba ya Bajeti ya Serikali. Kabla sijaanza, niseme tu kwamba Mheshimiwa Rais amejitahidi sana kufanya mabadiliko makubwa sana katika nchi yetu na baadhi ya mambo ambayo ameyafanya ambayo lazima tumshukuru na tuendelee kumuunga mkono ni mambo yafuatayo:-

Kwanza, suala la kuhamia Dodoma halikuwa jambo dogo kwa hiyo kwa nia hiyo njema ambayo Mheshimiwa Rais ameifanya kuhakikisha kwamba Makao Makuu ya Serikali yanahamia Dodoma na kufanikisha zoezi hilo baada ya miaka zaidi ya 40 ni jambo la kumshukuru sana na kumpongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine ambalo ni masuala ya usafirishaji. Zoezi hili la kuunda reli kwa kiwango cha standard gauge ni jambo ambalo lazima tuishukuru Serikali na tuendelee kuipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi ambazo wanaendelea kufanya kwa sababu ninaamini kabisa kama reli hii itakamilika ina maana uchumi wa nchi yetu utaboreshwa zaidi na hatimaye tunaweza tukapata mafanikio makubwa katika siku chache zijazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile amejitahidi sana kuhakikisha kwamba masuala ya watumishi hewa, wanafunzi hewa, manunuzi ya ndege, meli mbili lakini vile vile amerudisha nidhamu katika masuala mazima ya kazi. Haya ni mambo ambayo tulikuwa tukiyatamani na tumempata sasa kiongozi au Rais ambaye ameweza kweli kufanya mabadiliko makubwa katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze jambo moja ambalo limetokea kipindi kifupi kilichopita nalo ni kuhusu masuala la madini, masuala ambayo ni muhimu sana katika ujenzi wa Taifa letu. Suala la makinikia ni suala ambalo kweli ni la muhimu sana katika ujenzi wa Taifa letu. Tukiangalia kwa namna ambavyo Mheshimiwa Rais amejitahidi kulifuatilia na kulifanyia kazi suala hili na hatimae leo hii tunaenda kuunda sasa utaratibu mpya wa kuleta ule Muswada katika Bunge hili ili tuweze kuweka sheria ambayo itaweza kuhakikisha kwamba tatizo la madini katika nchi yetu linakwisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili sio jambo dogo, ni kweli kwamba katika nchi/mataifa mbalimbali mbalimbali wamejitahidi sana kufanya utaratibu wa kuja katika nchi maskini, kunyonya nchi maskini, kuchukua rasilimali zetu, kuondoka nazo na kutuachia na umaskini katika nchi yetu. Lakini tumempata Rais ambaye ameenda kufanya mabadiliko, amelichukua hili kama jambo lake, amelichukua hili kama jambo la Serikali na hatimae sasa kuwafanya Watanzania waanze kuanza maisha mapya kwa kuwa na imani na Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba jambo kama hili ni jambo ambalo linahitaji kwa ujumla wetu bila kujali upinzani, bila kujali Chama Tawala kuhakikisha kwamba tunamuunga mkono Rais katika kuhakikisha kwamba tunaleta maendeleo katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo niseme tu kwamba kwenye Bajeti ya Serikali, bajeti ya mwaka jana ilieleza kwa undani zaidi ikasema kwamba kuna zile dola milioni 500 ambazo zilikuwa zinatakiwa kutoka katika Serikali ya India ambazo zilikuwa zinalenga uboreshaji wa miundombinu ya maji katika nchi yetu. Lakini mpaka leo fedha hizo hazijatoka.

Ningependa kuishauri Serikali na kuendelea kuwashauri wadau ambao wako nje katika nchi ya India, wafanye kazi ya ziada, Serikali iendelee kusukuma, kutoa msukumo wa hali ya juu ili tuweze kupata fedha hizi ziweze kusambaa katika maeneo mbalimbali ya Taifa letu ili tatizo la maji sasa liweze kupungua. Tukiweza kufanya hivi tutapunguza adha ya maji katika Taifa letu.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna akina mama ambao wako vijijini, kuna watoto ambao wako vijijini, kuna shule na taasisi mbalimbali ambazo hazijafikiwa na huduma hii ya maji. Tukipata fedha hizi inakuwa inaleta sababu moja au maana moja kwamba tutapunguza adha ya maji katika maeneo mbalimbali hasa katika yale maeneo ya vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kwamba Taifa letu linapita katika wakati mgumu sana, wakati ambapo katika vijiji vyetu kila kona utakayoenda tatizo la maji litakuwa ndilo tatizo la kwanza kuzungumzwa. Lakini lazima tuendelee kuiwekea mkazo hii ya kwamba fedha ambazo zimewekwa katika Wizara au zimeombwa na Wizara husika Serikali iweze kupeleka fedha zile ili maji yaweze kutatuliwa kama changamoto kubwa katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba ongezeko la Deni la Taifa limekua. Lakini ni lazima tuangalie, je, ongezeko hili tunaweza tukalihimili au hatuwezi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokisema ni kitu kimoja, nchi mbalimbali katika dunia hii bado wanaendelea kukopa, wala isiwe shida kwamba Tanzania deni la nchi au Deni la Taifa limeendelea kuongezeka. Tuangalie nchi kama Marekani, tuangalie nchi zingine kama Kenya, tuangalie nchi zingine za Bara la Afrika, je, zinaendelea kukopa au haziendelea kukopa na je, katika suala la ukopaji tunakopa kwa ajili gani, hauwezi ukakopa bila kuwa na sababu maalum, na sisi tunavyoendelea kukopa isimaanishe kwamba Watanzania labda ni maskini, isimaanishe kwamba Watanzania hatuna mikakati ya namna gani tunaweza kukamilisha changamoto zetu za kimaendeleo, tunakopa kwa sababu tunataka tukamilishe miradi mbalimbali ya kimaendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapopata fedha hizi ina maana ni moja kwa moja tunaenda kuhudumia miradi mbalimbali katika vijiji vyetu katika miji yetu na kuhakikisha kwamba miundombinu ambayo tunaiona kwa mfano fly over tunazoziona Dar es Salaam, hii ni sababu mojawapo kwamba tunavyoendelea kukopa ina maana tunaboresha miundombinu yetu, kama tunatengeneza reli, barabara na miundombinu mingine yoyote ambayo tunaweza kuitamka, kama tutatumia fedha hizi kwa uangalifu na tukakopa kwa uangalifu basi wala isiwe shida kwa sababu deni hili ni sustainable.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mengi ya kuongea nijaribu kugusia tatizo moja la benki ya FBME ambayo miezi kama miwili iliyopita ilisimamishiwa leseni yake, niseme tu kwamba benki hii ni muhimu kwa wananchi, na kuna wateja ambao waliweka fedha zao katika benki ile. Imefika sasa wakati kwamba Serikali iweze kutoa tamko la moja kwa moja kwamba ni lini sasa fedha hizi ambazo wananchi au wateja ambao wapo katika benki hii wataenda sasa kuzipata, kwa sababu mpaka sasa hivi imekuwa kama ni dilemma, haieleweki kama Je, Serikali itatoa lini tamko kwamba leseni hii baada ya kufungiwa sasa wateja waende wapi kuchukua fedha zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchumi wa nchi yoyote na hasa uchumi katika mataifa madogo kama Tanzania ambayo yanategemea ukuaji wa mabenki, ambayo yanategemea ukuajia wa fedha ambazo zinakuwa deposited katika mabenki mbalimbali...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru sana naomba nichukue nafasi hii kuunga mkono hoja, nakushukuru sana Mungu akubariki. Ahsante sana.