Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kabla sijaanza naomba ninukuu maneno ya busara kabisa ya baba wetu wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwenye kitabu chake cha Freedom and Socialism.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ukurasa wa 32 anasema; for too long we in Africa and Tanzania as part of Africa we have slept and allowed the rest of the world to walk around and over us. Kwa tafsiri isiyo rasmi anasema; sisi Bara la Afrika na Tanzania tukiwa sehemu ya Afrika tumelala kwa kipindi kirefu wakati wenzetu wakitembea na wengine wakitembea hadi kwenye migongo yetu. Mwisho wa kunukuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Iringa kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwa Amiri Jeshi Mkuu wanchi hii ambaye hajalala na anaendelea kutuamsha Watanzania wote kuhakikisha hatupotezi rasilimali za Taifa hili. I know some people are still in denial, lakini kwa yaliyotokea juzi I am sure a lot of people are catching up. Najua tutafika, Mheshimiwa Rais tunakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo naomba nichukue fursa hii nikupongeze Mheshimiwa Waziri wa Fedha, baba yangu Mheshimiwa Mpango na dada yangu Mheshimiwa Ashatu kwa kutoa bajeti ambayo imetatua changamoto nyingi zilizokuwa zinawasumbua Watanzania. Nikupongeze kwakutoa tozo la kwenye mazao. Hii imewasaidia sanaespecially wanawake ambao ndiyo nguvukazi kubwa wanaojishirikisha na shughuli za kilimo. Kwa hilo nawapongezeni sana.

Vilevile nikupongeze kwa kuongeza hii tozo ya shilingi 40, lakini nakusihi Mheshimiwa Waziri wa Fedha, ili wananchi wasisikie uchungu wa tozo hii, tunaomba zitakapokusanywa tuhakikishe tunaenda kutatua zile kero ambazo zimekuwa zikiwasumbua muda mrefu especially issue ya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wangu wa Iringa bado tuna changamotokubwa ya maji. Maeneo ya kilolo kule Ilula bado ni changamoto kubwa, Mufindi, Mafinga bado ni changamoto kubwa, pale mjini kidogo wamejitahidi na Iringa Vijijini bado tuna changamoto ya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kuna jambo lingine ambalo ningependa niliongelee. Kwa mujibu wa Sheria ya Finance Bill ya 2016, tulitaka hawa operators wote wa simu walete hisa zao sokoni maana ya Dar es Salaam Stock Exchange. Lengo lilikuwa ni kuongeza transparency ili tujue ni nini kinaendelea kwenye haya makampuni.

Pili, tulitaka kuwapa fursa Watanzania ili waweze kushiriki moja kwa moja katika kumiliki uchumi wa nchi yao, haya ndiyo yalikuwa matarajio yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Vodacom walikwenda sokoni ili kutekeleza takwa hili la kisheria. Nikiuliza hapa Wabunge wangapi wamenunua hisa hizi they will be very few. Sasa kama muitikio huu umekuwa mdogo kwa Waheshimiwa Wabunge, imagine kwa mwananchi wa kawaida kule kijijini ambaye hajapewa elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kama ifuatavyo; wakati haya makampuni mengine yanajipanga kwenda sokoni sasa sisi ingebidi tuhakikishe tunatoa elimu kwa wananchi. Elimu ya kutosha na tusiwaachie makampuni ya simu peke yao. Sisi kama Serikali tuna taasisi nyingi ambazo ziko jirani na hawa wananchi zitaweza kutoa elimu juu ya umuhimu wa kumiliki hisa hizi. Sasa kwa sababu muitikio umekuwa mdogo basi tupunguze kutoka kwenye hii asilimia 25 tuanze asilimia10 mpaka15 then baade hali ikikaa vizuri tutarudi back to asilimia 25. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tushirikishe hata wenzetu kuna hawa East African Community,SADCna baadae hata iende dunia nzima kama wenzetu wa TBL na TCC walivyofanya. Nina uhakika hili jambo linawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa MWenyekiti, nina jambo lingine ambalo ningependa Mheshimiwa Waziri utakapokuja kumalizia hapa ulipatie kidogo ufafanuzi. Wenzetu wa Kenya, Serikali ya Kenya imefanya non tax barrier kwa wasambazaji na wasindikaji wa gesi ambayo inatumika nyumbani. Sasa hivi hawa wasambazaji kutoka Tanzania hawaruhusiwi kupeleka gesi hii nchini Kenya. Hii ni kinyume kabisa na matakwa ya East African Community. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi kama Wakenya wataendelea na msimamo huu na sisi tuzuie bidhaa zao kuingia nchini Tanzania. Ni nani haelewi ni kiasi gani Wakenya wame-benefit kutoka kwenye nchi hii? Leo Blue Band tunazotumia nyingi zinatoka Kenya, tukija kwenye maziwa, robo tatu ya maziwa ambayo yanaingia Tanzania yanatoka Kenya, madawa, sabuni zinatoka Kenya. Hii sio sahihi, natambua ushindani wa kiuchumi lazima uwepo na mimi hapa nilishauri lazima tu-send statement uwezo wa kuzalisha maziwa nchi hii tunao! Tuna ng’ombe wa kutosha, tuna viwanda vizuri vya kisasa. Iringa pale tuna kiwanda kikubwa cha Asas, nilisema last time kina uwezo wa ku-process lita laki moja kwa siku. Na pale Iringa kuna wananchi ambao maziwa yanaozea ndani. Nimekuwa naongea, tuwatengenezee miundombinu, collecton centres tuwape hawa wakusanye maziwa yaende kwa yule mwenye kiwanda pale. Tu-send statement kwa hawa Wakenya kuwa tuna uwezo wa kuendesha viwanda vya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri na tukiikubali hii habari ya gesi moja tutapoteza ajira, pili tutapoteza mapato. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri naomba hili jambo tulitolee ufafanuzi wa kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naendelea kukupongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, nawatakia heri katika utekelezaji wa bajeti hii. Nashukuru sana.