Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kupata fursa ya kuchangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango. Sisi kama Taifa tuna tatizo kubwa sana la kiuchumi yaani kwa lugha nyepesi tunaweza tukasema tuna economic crisis na ndiyo tatizo la ki-mindset kwa watu wote. Tatizo tulilonalo kama Taifa tunataka kutatua matatizo ya kiuchumi kwa majibu ya kisiasa, hilo ndilo tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana mapato kila siku yanashuka. Hata kule TRA mapato yanashuka mpaka



yameachwa kutangazwa sasa hivi. Lakini majibu yanayokuja ya kisiasa. Niseme tu kwamba hata bajeti ya mwaka 2017 ambayo sisi kama Wabunge hususan Wabunge wa Chama cha Mapinduzi tumekuwa tukiita ni bajeti ya kihistoria. Mimi nasema ni bajeti ile ile kwa sababu hakuna jambo jipya ambalo unaweza ukajifunza kwenye hii bajeti. Na niseme tu kwa mara ya kwanza hii bajeti ina tone ya kisiasa yaani siasa ni nyingi kuliko hali halisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukienda kwa huu utaratibu tutashindwa kupata suluhu ya tatizo na ndio maana siku mbili/ tatu uliona issue ya makinikia sasa badala ya ku-solve kitaalam suala la makinikia linatakiwa li-solve kisiasa kwa hiyo ikawa sasa politics inatawala kwenye jambo ambalo linatakiwa watu walijadili kitaalam, hilo ndilo tatizo tulilonalo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye bajeti karibu kila kitu ni kile kile, nchi za wenzentu kwa mfano nchi ya Kenya wanapoandika bajeti kama hii wanakukambia bajeti yetu kwa mwaka huu itapunguza tatizo la ajira kwa kiasi fulani. Sisi bajeti yetu imezungumzwa yote, lakini haikuambi mwaka huu wa fedha 2017/2018 tutapunguza ajira kwa kiwango gani. Majibu ni yale yale tatizo la kiuchumi linatafutiwa suluhu ya kisiasa. Hilo ndilo tatizo tunalokabiliana nalo. Bajeti za wenzetu inapojadili namna ya kupunguza umaskini inaeleza vizuri kabisa, bajeti ya mwaka huu shilingi trilioni 31 kwenye bajeti ya maendeleo shilingi trilioni 11 tutapunguza umasikini kwa kiwango cha asilimia moja, wenzetu wanaeleza bajeti hii haielezi, hata mpango wenyewe haulezi hauende direct kwenye haya mambo. Tatizo ni lile lile, matatizo ya kiuchumi tunataka kuyatatua kisiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu nchi nyingine Bunge halijadili madawati au sijui Halmashaluri yangu haina vyoo, hayo ni mambo yanayotakiwa yajadiliwe kwenye ngazi za Halmashaluri. Bunge tunatakiwa tuzungumze mambo makubwa sera za kiuchumi za kitaifa. Tuishauri Serikali namna ya kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, haya ndiyo mambo ambayo tunapaswa kuyajadili. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kitu kimoja, mwaka 2014 Katibu Mkuu wa CCM, Mheshimiwa Kinana alipokuwa Mbeya katika uwanja ule wa CCM akasema vizuri kabisa kwamba CCM tunapaswa kuwaomba radhi Watanzania kwa sababu tumewakosea sana. Haya maneno hata ukienda kwenye YouTube utaikuta ile hotuba ya Mheshimiwa Kinana alieleza vizuri sana kwa sababu alikuwa anajua na aliainisha kwa nini tuwaombe radhi Watanzania, sasa hapa hakuna kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii bajeti ya kihistoria, mimi nilijadili hapa namtafuta mtu maskini anaondokaje kwenye wimbi la umaskini, sioni, ndiyo zinaongezeka hizi sera. Wamekuja hapa na kufuta hiyo annual motor vehicle license ya shilingi 40 halafu unasema kwamba itaongeza tu shilingi bilioni 27.

TAARIFA

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kangi Lugola ni rafiki yangu wa karibu sana na anapozungumza kauli kama hizi unajua ukimjibu kisiasa atapotea kabisa kwa sababu nchi hii tumeshawahi kuwa na Rais Mwamba wa Afrika, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sasa ukisema Nyerere unaweza ukamtoa kwenye hiyo reli unakuwa unakosea sana na siyo majibu mazuri. Akumbuke vizuri kabisa kwamba wapo akina Mkapa na Kikwete hatujawahi kupuuza mchango wao pamoja na kwamba wamewahi kuwa na makosa. Kwa hiyo, ni vizuri Mheshimiwa Kangi ukatambua mchango wa wale wazee wengine maana yake wakikusikia wewe uliyekuwa unawaunga mkono leo ni kama vile unaona hawakuwepo, siyo jambo jema kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuna shida na uwepo wa Rais Magufuli, hatuna shida na jambo hilo lakini tunachokijadili, tunajadili ni namna gani Chama cha Mapinduzi kinavyotekeleza hizi sera ambazo hazitekelezeki. Unajua kuna kitu kimoja watu wanasema ametoka Kikwete amekuja Magufuli lakini wote wanatekeleza Ilani ya chama kimoja. Magufuli hatekelezi sera za kwake binafsi, anatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ndivyo alivyofanya Kikwete, Mkapa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa huwezi kuwatofautisha Magufuli na Chama cha Mapinduzi ama Kikwete na Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo, jibu jepesi ni kwamba Serikali iliyokuwepo madarakani kwa kipindi chote ni ya chama kimoja ya Chama cha Mapinduzi tu. Kwa hiyo, makosa yote ambayo tunayataja yameletwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi, hicho ndicho tunachokijadili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nieleze tu vizuri kwamba tunahitaji kujadili mambo ya msingi, kwa mfano Waziri wa Fedha hapa amekuja ameongeza shilingi 40, kuna watu wameeleza hapa wanaona kama vile ni kisenti kidogo lakini cha ajabu sisi tume-question pale unaongeza shilingi 40 kwenye mafuta ya taa, hebu Mheshimiwa Waziri wa Fedha nieleze kwenu Buhigwe ni gari gani inatumia mafuta ya taa

ama kuna Bajaji inatumia mafuta ya taa yaani unakuta hakuna majibu. Sasa of all kwenye ile lita moja ya mafuta ya taa bado Serikali inapata shilingi 425, tozo inatoka pale. Kwa hiyo, ukiongeza shilingi 40 maana yake mwananchi wa kijijini atalipa tena shilingi 465 nyingine, sasa hayo ni maswali ambayo tunapaswa kujiuliza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda watu hawajui, kwa siku sisi kama Taifa tunatumia lita 8,300,000; lita 5,000,000 zinatumika kwenye mafuta ya dizeli, lita 3,000,000 tunatumia kwa ajili ya mafuta petroli na lita 300,000 yanatumika kwenye mafuta ya taa. Sasa jaribuni kukokotoa ndiyo mtajua kiwango ambacho kinakwenda kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuli-propose hata kwenye Kamati hata Mheshimiwa Waziri wa Fedha anaweza kujua, tulisema ni bora ikaongezeka shilingi 50 kwenye mafuta iende kwenye maji ili wananchi wa vijijini wapate maji kwa sababu tatizo la nchi hii ni maji. Waziri akakataa akasema hiyo Sh.50 ikiongezeka itaongeza gharama ya mafuta na wananchi maskini watapata shida. Sasa leo kafanya kitu kile kile kwenye angle nyingine, sasa maana yake ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine ni kutokuaminika, sijui ni kutojielewa au kijichanganya, hayo ndiyo mambo ambayo sisi siku zote tumekuwa tukiyapinga na tunalieleza Bunge lijaribu kuyaangalia. Ingekuwa vizuri sisi kama Bunge kwa umoja wetu tukakubaliana hapa kwamba pamoja na kwamba motor vehicle imefutwa, kwa kifupi siyo kwamba imefutwa isipokuwa tumebadilisha tu utaratibu wa kulipa. Kufuta maana yake hicho kitu hakitakiwi kuonekana mahali popote, ni kwamba tumebadilisha kutoka kulipa direct inakwenda kulipwa indirect, mfumo ni ule ule yaani kupunguza maumivu ya namna ya kulipa, haijafutwa. Ieleweke vizuri haijafutwa ila tumebadilisha utaratibu, kama ni kufuta unaoindoa pale.

Sasa hii shilingi 40 kama Bunge tuidhinishe humu ndani iende kwenye miradi ya maji vijijini ili wananchi wote wapate maji safi na salama lakini ikienda huko huko itaishia tu kuwa katika matumizi ya kawaida na mwisho wa siku haitafanya jambo lolote la msingi kwenye bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa angalia trend za bajeti zote za miradi ya maendeleo, kwa miaka nenda rudi bajeti za miradi ya maendeleo zimekuwa zikitekelezwa kwa kiwango kile kile chini ya asilimia 40. Sasa leo unapokuja na bajeti ya tone ya namna hii, mwakani sisi tutakuhoji tu vilevile. Maana yake hapa tumeficha uso wetu kwamba mwaka jana ni kama vile hakukuwa na jambo lolote lililofanyika lakini ukweli mwaka jana Wizara ya Fedha na Mipango mmefeli kwa kiwango kikubwa tofauti na matarajio ambayo tulikuwa nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, alipokuja bajeti ya mwaka jana Mheshimiwa Waziri akajisifu akasema mimi ni ndiyo nimeingia, nisikilizeni, mambo yatakavyokuwa motomoto basi sisi tukakosa mpaka hoja, iwe ni Wapinzani na Chama Tawala tukakaa kimya tukasema ngoja tusubiri kinachokuja, kilichotokea ni nini? Ni yale yale ambayo miaka ya nyuma yamekuwa yakifanyika, utekelezaji wa bajeti ya maendeleo upo chini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeomba Serikali itakapokuja kuhitimisha ituonyeshe namna gani inaweza kutekeleza ile bajeti yake ya miradi ya maendeleo na iainishe vyanzo vipya. Kitu kingine tunakushauri chukua kwenye bajeti yetu mbadala, kuna vyanzo tumekushauri ikiwemo Euro Bond, float Euro Bond utapata karibu shilingi trilioni 2.2 itakusaidia kwenye kutekeleza miradi ya maendeleo. Ni ushauri wa bure ambao kama ukitaka unaweza kuchukua na usipotaka basi lakini kwa maslahi ya Taifa, ahsante sana.