Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba niungane na Waheshimiwa Wabunge wote, wanaompongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri sana anayoifanya kwa Watanzania.

Pili, nipongeze sana Serikali kwa kuleta mpango huu na bajeti hii ya mwaka 2017/2018. Ni bajeti ya kipekee sana ambayo inagusa maeneo yote makubwa ambayo kama ya tatekelezwa vizuri, yatawatoa Watanzania na kuwafikisha kwenye uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maslahi ya muda, kwanza niishukuru sana Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa kuitazama kwa namna ya pekee sana Halmashauri yetu ya Wilaya ya Madaba na Jimbo la Madaba. Kimsingi kushukuru ni kuomba tena, wana Madaba katika kipindi hiki cha mwaka mmoja, tumeona maendeleo makubwa sana katika maeneo mbalimbali ikiwemo afya, maji, nishati na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawashukuru sana Waheshimiwa Mawaziri na Wizara zenu, lakini zaidi Mheshimiwa Rais ambaye amewakabidhi haya majukumu. Wana Madaba tunatambua mchango mkubwa wa Serikali kwa maendeleo yetu na ninaamini tutaendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali hii kwa sababu tunaamini ndani ya kipindi cha miaka mitano wana Madaba tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana ya kimaendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango mkubwa ambao nilitaka niutoe kwako na kwa Wabunge leo hasa kwa Serikali, ni mahusiano ya kilimo na Tanzania ya viwanda. Kwa Muktadha wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015/2020. Ukitazama katika Ilani yetu, kipaumbele cha Awamu ya Tano ni kuwa na viwanda Tanzania nzima ili kutoa ajira kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sehemu kubwa Serikali imeweka misingi imara ya kutengeneza au yakujenga Tanzania ya viwanda. Miaka miwili tu baada ya kuanza Serikali hii au mwaka mmoja na nusu, tayari tunaona viwanda vingi vinajengwa. Hata hivyo ninaomba niikumbushe Wizara na niikumbushe Serikali kwamba aina ya viwanda vinavyojengwa, pamoja na kwamba ni viwanda vizuri, lakini aina hii bado haiendi kujibu kwa namna inavyotakiwa mahitaji makubwa ya Watanzania wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ilani ya Chama cha Mapinduzi, inatutaka aina ya viwanda ambavyo vinatakiwa tuvijenge sana ni vile ambavyo vitaongeza thamani ya mazao yetu na hivi kutoa soko na kuongeza kipato kwa mwananchi mkulima.

Tukumbuke kwamba Watanzania asilimia 80 tunaishi kwa kutegemea kilimo, tunategemea masoko mazuri ya kilimo na masoko haya tutayapata tu iwapo tutafanikiwa katika Serikali ya viwanda. Tutajenga viwanda vya kusindika mahindi, pamba, ufuta, alizeti, tangawizi na kadhalika. Hilo ninaliona hatujalifanyia kazi kwa namna ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, unaona kwamba mahitaji ya mafuta ya kula peke yake ni lita 400,000, hizi ni sawa na alizeti tani milioni mbili tu. Na hizi tani milioni mbili wana uwezo wa kuzalisha wakulima 4,000 tu, wanaweza kuzalisha mafuta yote ya kula…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila mpangilio)

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kiasi hiki, hizi lita za mafuta laki nne wanaweza kuzalisha wakulima 4,000 tu iwapo watajengewa uwezo. Lakini inasikitisha kuona hadi leo asilimia 70 ya mafuta ya kula tunaagiza kutoka nje, wakati wakulima wengi hawana fursa ya kuzalisha na kuuza kwa bei nzuri mazao yao kilimo, kwa hilo ni tatizo. Tatizo hili linatoka wapi...(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzunguzaji)