Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na mimi kwa kuweza kupata nafasi kuchangia katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Cha kwanza kabisa naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Waziri, pili naunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuiongoza nchi hii kwa umakini kabisa na kwa uhodari mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, nilitaka kuweka jambo moja sawa kwamba bajeti inakua, bajeti haiwezi kusimama hapo hapo, bajeti lazima ikue. Ili bajeti iweze kukua kuna mikakati ambayo inakua imewekwa. Kwa mfano tumeweka mazingira mazuri ya kujenga viwanda, na viwanda vinajengwa na wadau mbalimbali Serikali haijengi viwanda. Vilevile mmeona tunatengeneza miundombinu, miundombinu ikikaa sawa ina uhusiano wa moja kwa moja. Tumegusa suala la kilimo, kilimo pia kitasaidia kuleta malighafi katika viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie suala lingine la kusema kwamba CCM itaondoka madarakani, lakini siku chache zilizopita TWAWEZA wametoa takwimu hapa, wameonesha nani anapanda, nani anashuka. Mimi sipendi kuingia huko lakini TWAWEZA wameweza kutuonesha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia suala zima la bajeti sasa katika mchango wangu, bajeti ni shilingi trilioni 31, lakini kodi ni shilingi milioni 17 na tax revenue shilingi trilioni mbili na madeni ni shilingi trilioni 11 ndipo tunafika kwenye shilingi trilioni 31 maana yake nini? maana yake ni lazima tuangalie vyanzo vipya vya mapato. Na vyanzo vipywa vya mapato vya haraka haraka lazima informal sector, World Development Report ya mwaka 2017 inazungumza kwamba katika nchi zinazoendelea, informal sector ina-constitute karibu asilimia 40; sasa lazima tuangalie hiyo informal sector tutaileta vipi kwenye net ya kulipa kodi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo maeneo machache ambayo pia yanatakiwa yaangaliwe, consultancy. Watu wanafanya consultancy lakini hawalipi kodi, lakini kuna watu wanafanya kazi mbili/mbili hawalipi kodi lakini pia Rais amesema mikataba itakuja ya madini, mikataba ya madini ikija itaongeza kipato, na hiyo inajibu hoja ya kusema hatukuweza kukusanya vya kutosha, hatuku-perform vizuri. Pesa zinakuja, pesa zikija tutaweza kuigharamia bajeti yetu bila tatizo lolote lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hayo lazima sote na Waziri atambue kwamba tumeweka mpango na lazima pesa zipatikane, kwa hiyo, pesa zitapatikana kwa kuweka mikakati mizuri na pesa zikipatikana mimi nina uhakika kabisa hata Jimbo langu la Mkalama Daraja la Sibiti litakamilika, barabara zitakamilika, huduma ya afya itakuwa sawa na maji watu watakunywa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la motor vehicle. Tumeondoa motor vehicle, tumeweka utaratibu huo mzuri wa shilingi 40. Hiyo shilingi 40 tupige hesabu tuone kwamba tulitakiwa tukusanye pesa ngapi kama tusingeondoa motor vehicle. Kwa hiyo pesa iliyozidi ambayo mimi nimepiga hesabu hiyo pesa imezidi imepelekwe kwenye maji iwe refenced, ichangie kwenye mfuko wa maji itakuwa ni jambo zuri.

Niende kwenye suala la madini. Tumezungumzia suala la gypsum nazungumza suala la gypsum kwa sababu kule kwangu Dominiki gypsum ipo. Nashukuru Serikali kwa kuona viwanda vya ndani kutumia gypsum ya hapa kwetu, lakini basi uwekwe utaratibu mzuri wananchi wawezeshwe. Hiyo gypsum mimi niliangalia haina utaalam sana wa kuchimba, kwa hiyo, kama Wizara ya Madini na Nishati itawawezesha wananchi kuweza kuchimba hiyo gypsum wenyewe na masoko ambayo tunayajua wananchi watanufaika. Pia wale maofisa wa madini wanatoa leseni tu wananchi wanakwenda kuondolewa bila utaratibu wowote, hilo jambo liangaliwe na huko wananchi wanaweza kunufaika na madini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao chini ya tani moja. Tumesema kwamba mazao chini ya tani moja yasilipiwe ushuru wowote. Hapa yako mambo mawili, kwanza tunaipongeza Serikali kwa hatua hiyo lakini tutambue kwamba wako wafanyabiashara wajanja, walanguzi ambao wanaweza wakatumia mwanya huo kupoteza mapato hayo. Sasa viwekwe vituo vya kuuzia mazao, kwa hiyo, Halmashauri wapewe leseni za kununua mazao kwenye vituo maalum tusiruhusu walanguzi kuingia kwa wananchi na yenyewe itakuwa ni jambo litakalosaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tujue kwamba sasa Halmashauri zitapoteza mapato, kwa hiyo tukadirie tuone kwamba mapato yatapotea kiasi gani na tuone hizi Halmashauri zitafidiwa kiasi gani. Kwa mfano, sisi Mkalama zile own source kubwa zinategemea hizi kodi……..

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji