Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaomba nijibu hoja ambayo imejitokeza hapa inasema kwa nini hatupongezi.

Kwenye hesabu ya form five na six au wale ambao mmesoma Additional Mathematics kuna topic inaitwa Logic, yaani kama una true/false maana yake ni false, kama una false/ true unapata ni false, kama una true/true ni true. Sasa sisi hatupongezi wala hatuungi mkono hii bajeti kwa sababu nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, kwenye bajeti ya mwaka 2016/2017 Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ilipata fedha asilimia 18 tu, tunapongezaje hapa? Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni asilimia 3.31, unapongeza nini? Wizara ya Maji na Umwagiliaji ni asilimia 8.4, unapongeza nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mmezungumza habari ya madini hapa mnataka sisi tupongeze lakini mikataba hatujaiona, misamaha mliyotoa hatujui, wahusika hawajashughulikiwa, mchanga ndiyo umezuiliwa, dhahabu inaendelea kuzolewa, Wanyamongo pale Tarime wanapigwa wapo ndani wamevunjwavunjwa, tuna makaburi mengi, tuna makovu, kuna watu ambao hawawezi kuzaa kwa sababu wamekunywa sumu madini ya zebaki, tunapongezaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja wapo ya sababu ambazo Mheshimiwa Waziri ametaja ya bajeti kutotekelezwa, ametaja Afrika kwamba uchumi haujakua kwa sababu ya utawala bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kule Mawazo Katoro amenyongwa mchana kweupe, alikuwa kijana wetu wa Upinzani, wa CHADEMA, ameuawa katika utawala huu, tunapongeza nini? Tunapozungumza, Ben Saanane hayupo na Serikali haitoi majibu, huyu ni kijana Mtanzania mzalendo, tunapongeza nini?

T A A R I F A .....

HE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, imepita kama upepo, yaani siipokei, siikubali, ndiyo utaratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee. Viongozi wa Serikali na Chama Tawala ni muhimu mkawa makini sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasema tu kwamba naomba muda wangu ulindwe. Mnapotaka tujadili kama Taifa, kama Bunge moja ni muhimu pia tukaangalia vipande vipande vya matukio mbalimbali. Kwa mfano mmeteua watu ambao wanaiwakilisha Serikali katika maeneo mbalimbali, lakini tunapozungumza hapa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai anazuiliwa kufanya kikao cha halmashauri, Mstahiki Meya wa Ubungo yupo ndani, amewekwa lock up. Tunapozungumza Mkuu wa Wilaya anaongoza wenzake na Jeshi la Polisi ambalo tunalipa kodi kuwapa mishahara na nguo na kila kitu, wanakwenda kuharibu shamba la Mtanzania mmoja amewekeza, Mheshimiwa Mbowe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wakati mwingine mnaposema tuungane mkono kwa kweli tunashindwa kuwaelewa, haya mambo tunayounganisha, connectivity, inakuwaje? Kwa sababu kama mnataka tuungane katika mambo ya msingi, humu ndani kwenye Bunge hili wenzetu akina Mheshimiwa Halima Mdee, Mheshimiwa Ester Bulaya wamewajibishwa hapa kwa adhabu kubwa kubwa. Juzi umeombwa mwongozo mtu anaomba mwongozo, Mwenyekiti anasimama anasoma mpaka vifungu, maana yake hilo jambo limeandaliwa limeandikwa. Sasa mnaposema tuunge mkono ni muhimu sana tukubaliane tunataka tufanye kitu gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa nini hatuungi mkono, kwa mfano Mheshimiwa Dkt. Mpango; mjukuu wangu wala sina shida na yeye; Mheshimiwa Dokta Mpango kwenye ukurasa wa 19, watu 7,277 wamefunga biashara zao. Hawa walikuwa wanasomesha, wana wagonjwa, wana watoto, wana kodi wanalipa maana yake zote zime-paralyze sasa unaungaje mkono, hili ni jambo kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kodi ya majengo, sisi kule Dar es Salaam pamoja na kwamba kuna ufugaji mdogo mdogo, kodi ya majengo tulikuwa tunapata shilingi bilioni 18 kwa mwaka kwenye taarifa hapa, Serikali kupitia TRA imekusanya shilingi bilioni 15, Mkoa wa Dar es Salaam peke yake ni shilingi bilioni tisa, unapigaje makofi katika eneo hili? Halmashauri imeondolewa kukusanya kodi, Halmashauri imenyang’anywa… (Makofi)

T A A R I F A

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Huyu ni Mbunge wa kule Tabora, Wilaya yake ni maskini kweli kweli, kwa hiyo nadhani tutafute hela hapa, yule nimefika kwake Sikonge haki ya Mungu hana hata lami yule, acheni kupiga makofi ya kishamba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasema, mimi naangalia upande wa negative, kwamba hawa watu walivyoacha biashara, imewa-affect, hii kama wamefungua au wamenufaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine, nimesema kule kwenye halmashauri hizi Wabunge wanapiga makofi sana lakini najua hii bajeti ikiisha mwaka ujao kila mtu atakuwa analia na kusaga meno hapa kwa sababu Halmashauri nyingi zinatumia kodi ya majengo, imenyang’anywa ilikuwa hata mabango, yamechuliwa asilimia tano akina mama na asilimia tano vijana, tunakwenda kuwakopesha nini? Kwa hiyo, Mheshimiwa Dkt. Mpango lazima aje na utaratibu wa kufanya replacement ya fedha ambayo imeondolewa halmashauri ili Halmashauri iweze kujiendesha. Mvua ikinyesha kidogo tu Halmashauri nyingi hazipitiki, hakuna miradi ya maji, tunasema halmashauri. Mheshimiwa Waziri alipoulizwa swali hapa anasema Mbunge ni Diwani aende kwenye Halmashauri wakae wajadiliane, mnajadili nini kama fedha hazipo? Mnajadili nini kama vyanzo vya fedha vimeshanyang’anywa? Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo ni muhimu mkaangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri amekuja na hoja, kwenye halmashauri zetu ilikuwa mtu akifanya kosa dogo anapigwa faini shilingi 50,000, imepanda mpaka shilingi 200,000 mpaka 1,000,000, mwaka mmoja mpaka miaka miwili, sasa hawa wananchi wa kawaida ambao ni maskini tunaowatetea tunawatengenezea adhabu kubwa na vifungo. Badala ya kuwaelekeza na kuwafundisha namna ya kufuata sheria tunatunga sheria za kwenda kuwakandamiza wakafungwe zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesema Machinga waende wakajiandikishe, ni jambo zuri zaidi, lakini eti ambaye hakujiandikisha atafungwa sasa mechanism ikoje kuwatambua hawa watu? Nani anafanya utaratibu huo ili akwame? Nadhani tungeelekeza nguvu kufundisha watu wetu na kuwaelekeza kufuata sheria, tusiende sana kwenye adhabu mbalimbali ambazo zinakwenda kuumiza watu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii bajeti Mheshimiwa Waziri hatuungi mkono kwa sababu gani, mlikujaa na bajeti ya shilingi trilioni 29 ya mwaka jana imekamilika kwa asilimia 38 tu. Umeongeza sasa unazungumza shilingi trilioni 31.4 haujaeleza ni miujiza gani itatumika fedha hii ipatikane. (Makofi)



Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri anakaa kule Zingiziwa kwangu kule Ukonga, unafahamu mvua imenyesha kwako huwezi kwenda kuna mahandaki, hakuna maji, nimenunua mpaka jenereta kule Zingiziwa shule ya Msingi kule ni Dar es salaam sasa kule kwenu kule Buyungu, Kakonko ikoje hali hiyo? Haya mambo ukiyalinganisha huwezi kupiga makofi humu ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnataka tujadili kama Taifa ni muhimu sana tukubaliane, mnavyotenda mtende kwa Watanzania wenzenu sawa sawa mnavyotendewa nyie, tuheshimiane. Kwanza utaratibu wa kuonyesha kwamba eti mtu akishakuwa mpinzani siyo Mtanzania sio sawa sawa. Hauwezi kutudharau kwenye mikutano, mkatunyima nafasi, tv mnatumia mnavyotaka nyie, inakua Chama tawala halafu tukija hapa tupige makofi. Mkiboresha mambo hayo sisi hatuna shida na ninyi na hakuna mtu ambaye anasema tuibiwe, sisi huwa tunapinga kuliko ninyi kwamba wizi mwiko. Leteni mikataba, Twiga walioibiwa, tubadilishe sheria, watu wanyongwe, watu wafilisiwe; na uzuri wa Mungu wote watakuwa Chama cha Mapinduzi hakuna mpinzani hata mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo vipi? Nakushukuru sana, siungi mkono hoja, ahsanteni sana.