Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niungane na Waheshimiwa Wabunge ambao wametangulia kusema kuunga mkono na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa hatua anazochukua katika ulinzi wa rasilimali zetu. Kazi anayoifanya ni kubwa, kazi hii inahitaji uthubutu mkubwa na kazi hii ni ya kizalendo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunachotakiwa kukifanya wote kwa umoja wetu tunaomba tumuunge mkono Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya. (Makofi)



Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili kama anvyoomba yeye mwenyewe, tuendelee kumuombea katika sala zetu ili aweze kuendelea kutekeleza majukumu yake na hatimaye ahamie kwenye sekta ndogo zingine hata sekta za gesi, utalii na maeneo mengine ambapo kunahitaji usimamizi madhubuti ili kuweza kuleta tija katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili niungane na wenzangu kumpongeza Waziri kwa kazi nzuri aliyoifanya, Mheshimiwa Dkt. Mpango na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji na wataalam wa Wizara hii wakiongozwa na Ndugu Dotto na Gavana wa Benki Kuu Profesa Ndullu. Tunaona kabisa waziwazi kwamba utaalam wao na weledi wao unasaidia sasa kuja na sera za kifedha ambazo zinasaidia katika uchumi wa nchi yetu. Kama takwimu zinavyoonesha kwamba uchumi wa nchi yetu unaendelea kupanda na kuimarika kwa asilimia saba kila mwaka, kwa hiyo tunakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, udhibiti wa mfumuko wa bei tumeona kwamba muda mrefu mfumuko wa bei bado uko kwenye digit moja. Siyo hivyo tu, pamoja na takwimu zinazotolewa kwamba kuna biashara zinaendelea kufungwa lakini kwenye kitabu cha Waziri hapa imeonesha wazi kwamba kuna biashara mpya zaidi ya laki 224,000 zimefunguliwa. Vilevile kitabu kimeonesha takwimu kwamba sasa pato la kila Mtanzania yaani per capita income imeongezeka kutoka milioni 1.9 mpaka milioni 2.1. Kwa kweli wanastahili hongera, bila usimamizi wa Waziri na watendaji wakuu haya yote yasingetokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nikupongeze vilevile kwa kuja na kitabu chako ambacho kimejibu hoja nyingi za wananchi na za Wabunge. Utakumbuka mwaka jana hapa uliambiwa kwamba wewe huna jimbo na una mpiga kura mmoja, lakini maneno hayo mwaka huu yote tumeyafuta, kwa hiyo, tunakupongeza sana kwa usikivu wako na kwa kweli Wabunge tunakupongeza kwa sababu mimi kila nikiangalia ukurasa, naona unajibu hoja ya Mbunge au unajibu kero za wananchi. (Makofi)



Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo naomba nitoe mchango wangu kuhusu mambo matatu, suala la kwanza ni hii ukurasa wa 48 umezungumzia hatua za mapato na hapa umezungumzia kuwatambua rasmi wafanyabiasha wadogo wadogo wasio rasmi na wanaofanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi, mama lishe, wauza mitumba, wauza mazao ya kilimo wadogo wadogo, mboga mboga na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki ni kitendo kibubwa sana kwa sababu mara nyingi kundi hili lilionekana kwamba halina msaada na halina nafasi katika uchumi wa nchi yetu. Kwa hiyo, tendo la kuwatambua na kuwasajili hii inaonekana wazi kwamba hawa sasa ni wadau wa maendeleo ya nchi yetu. Nishauri sasa kwamba kinachotakiwa kufanya sasa hivi ni kwamba Mamlaka ya Serikali za Mitaa basi zishirikiane na watu hawa yaani mipango ya kuwatambua na kuwatafutia maeneo iwe shirikishi tusiwe na ule utaribu kila siku tunawafukuza watambuliwe, wawekwe kwenye maeneo rasmi na tusahau ile miradi ya zamani, nafikiri wote tuna historia ya mradi ule wa Machinga Complex na lile soko la Mchikichini nini kinaendelea ni kwa sababu hatukuwashirikisha. (Makofi)

Kwa hiyo, kwa tendo hili ambalo sasa hivi tunaenda kuwatambua tuwasajili hii itasaidia sasa kuwapa maeneo ambayo yatakuwa karibu na wateja wao na maeneo yao ya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa pili sehemu ya pili ni ile suala kupunguza Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vyakula vya mifugo, lakini vilevile ni kupunguza Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa mayai ya kutotoa vifaranga hii itaongeza ajira kwa vijana wetu, kwasababu kuna vikundi vingi vya kinamama na vijana wanashughulika na ufugaji kwahiyo tukifanya hivi tutaongeza ajira kwa vijana wetu. Tunachotakiwa kutoa ushauri kwa mambo mawili kwamba tupunguze kodi ya madawa ya mifugo, lakini pili vikundi hivi vya vijana na kinamama sasa iweze kupewa mkopo ili waweze kufuga vizuri. (Makofi)



Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya tatu naenda kwenye sekta ya kilimo. Sekta ya kilimo nako kuna unafuu umepatikana kwa kupunza tozo mbalimbali kwa wakulima. Lakini kwa kipekee niishukuru Serikali kwa uamauzi wao kwa kuamua kugawa pembejeo za kilimo bure kwa wakulima wa korosho nawapongeza sana, lakini kwenye korosho bado tunatakiwa twende mbele zaidi tujikite katika ubanguaji wa korosho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakosa fedha nyingi sana tuna viwanda vya kubangua korosho 12; lakini kwenye mpango wetu tunazungumzia viwanda viwili tu. Kuna viwanda vingine kumi hebu tuviwekee mkakati ili tupate fedha nyingi lakini vilevile tutaongeza ajira kwa wananchi wetu, na wenzetu wa Msumbiji wana-practice policy, korosho nyingi za Msumbiji zinabanguliwa kwa nini sisi Tanzania tusibangue, kwa hiyo naomba sasa tujikite katika ubanguaji wa korosho ili tuache kuuza korosho ghafi nchi za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu mwingine ni utekelezaji wa miradi. Inaonekana miradi yetu inachukua muda mrefu sana kwenye utekelezaji kuna mradi huu wa miradi 17 ambayo inagusa Muheza, mradi wa Makonde, kuna mradi wa Njombe, miradi hii inatakiwa kuanza kutekeleza…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.