Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nichangie kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri waliyofanya. Kwa kiasi kikubwa Mheshimiwa Waziri mmejitahidi kusikiliza kelele za Wabunge hapa na ambao ndio wawakilishi wa wananchi na kwa kweli bajeti hii kwa kiasi fulani na kwa kiasi kikubwa ime-reflect ambacho tulikuwa tukikipigia kelele. Kwa hiyo, nadhani ni mfano mzuri wa Serikali kuwa sikivu kwa wale ambao inawasimamia hongera sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayofanya na hasa kwenye usimamizi wa rasilimali za nchi yetu. Nadhani ameonyesha mfano mzuri na kwa mjadala unavyoenda nadhani watu wengi wanamuunga mkono, wanaweza kupatikana wachache ambao pengine wana mawazo tofauti, lakini hiyo haitufanyi tusisonge mbele na msimamo wa kulinda rasilimali za nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ambalo ningelipenda kulisema katika hili nadhani ni vizuri ukweli huu ukasemwa kwamba hizi juhudi za kulinda rasimali za nchi yetu hazijaanzwa na Awamu ya Tano, zimeaanzwa kutoka Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Nyerere kuna mambo aliyafanya katika kuhakikisha rasilimali za nchi yetu zinalindwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mambo aliyafanya hata kama kunaweza kuwa na mapungufu. Awamu ya Pili ya Mzee Mwinyi yako mambo aliyafanya, Awamu ya Tatu ya Mzee Mkapa yako mambo aliyafanya, Awamu ya Nne ya Mheshimiwa Kikwete yako mambo aliyafanya mazuri. Kwa hiyo, hakuna namna ambayo tutapuuza juhudi zilizofanywa na watangulizi wa Mheshimiwa Magufuli, kwa sababu nao wana mchango hata kama leo yataonekana yalikuwepo mapungufu lakini kwa nafasi yao walitimiza wajibu wao. Na ni vizuri tukatambua mchango wao na kuuheshimu mchango wao badala ya kubaki tunawanyooshea vidole kama vile hawakufanya lolote kabisa katika juhudi za kulinda rasilimali za nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukisoma Ilani zote za Uchaguzi za Chama cha Mapinduzi, tumezungumza habari ya ulindaji wa rasilimali zetu. Kwa hiyo, hiki anachokifanya Rais anatekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ambayo ndio mkataba wa CCM na wananchi tukiunda Serikali. Hapa nitanukuu Ilani ya Uchaguzi inasema hivi; “kubuni na kutekeleza mikakati mahsusi itakayowezesha kupunguza au kukomesha kabisa vitendo vya utoroshaji wa madini kwenda nje ya nchi na biashara haramu ya madini nchi.” Kwa hiyo, iko kwenye Ilani ukisoma mwongozo, ukisoma muelekeo wa sera kote tumezungumza. Alilolifanya Rais Magufuli ambalo ndilo tunalomuunga nalo mkono
ametupeleka kwenye hatua kubwa zaidi ukilinganisha na hatua tulizozichua mwanzoni. Lakini anajenga kwenye msingi ambao ulishaanzwa na wenzake, kwa hiyo, kwa kweli tusitenganishe na kufanya kama vile waliopita ni waharifu hivi, hapana. Naamini walitimiza wajibu wao Magufuli anatimiza wajibu wake tumuunge mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na katika hili tunaweza tukagawanyika katika mitazamo, wapo wale wanaunga mkono asilimia 100, wapo wale wanaopinga kwa namna wanavyowaza wao. Sasa kelele zisiturudishe nyuma lazima tusonge mbele kwa sababu vita hii ni takatifu, lakini tusipuuze katika kelele nyingi kunaweza kuwa na ushauri mzuri ndani yake. Tusifike mahali tukapuuza kabisa nadhani sio jambo jema, hii vita ni yakwetu wote nchi hii ikifaidika na jambo hii ni faida kwetu wote bila kujali itikadi zetu za vyama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tusitoboane macho, tusitupiane vijembe visivyokuwa na sababu ni wakati wa kuileta nchi yetu pamoja twende tukapigane hii vita tuishinde. Kwa hiyo, wapinzani na CCM na watu wengine wote kwa ujumla wetu bila kujali tofauti zetu nadhani ni vizuri tukaungana katika hili, tuondoe tofauti zetu tusitafute mchawi kati yetu wenyewe sisi tuungane. Kama vita yoyote safari yoyote inaweza kuwa na mashimo na mabonde kunaweza kuwa na ghrama za vita hii, tukubali kuzilipa faida yake ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Rais kwa kazi hii na nadhani sasa ni wakati mzuri tumuunge mkono kama yako maeneo ya kurekebisha, kushauri tushauriane ili vita iishe salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili, ambalo nilitaka nilizungumzie Mhehimiwa Waziri uchumi wa gesi na mafuta. Sisi Kusini, Mikoa ya Lindi na Mtwara gesi na mafuta ndio ilikuwa inazungumzwa kuwa ni ukombozi. Bahati mbaya ugunduzi ulipopatikana habari zilizotolewa ni kama vile ndio tunageuza siku moja kule kuwa nchi ya asali na maziwa. Na ninyi mnajua habari ilipotoka kukatokea vurugu kubwa sana Lindi na Mtwara, kwa sababu habari iliyopelekwa kwa wananchi ilijaa chumvi nyingi badala ya kupeleka ukweli kwamba faida ya gesi yenyewe iliyogunduliwa na mafuta inaweza ikatuchukua zaidi ya miaka 20, 30 kabla hatujaanza kuifaidi. (Makofi)

Kwa hiyo, wako wananchi waliokata mikorosho yao wakiaamini biashara imeisha, wako watu waliokaa na kubweteka wakadhani mambo yameisha. Sasa nadhani hili lilikuwa kosa moja kubwa sana ndio maana ikatokea vurugu ya Lindi na Mtwara juu ya gesi na bomba lake na mambo yote yaliyoendana na hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sisi tulidhani kwamba mchakato kuelekea huko kwenye kufaidika ungeenda vizuri na kwa wakati. Na hapa nataka nizungumzie ujenzi wa mtambo wa kuchakata gesi (LNG plant) pale Lindi. Kwetu sisi huu ndio ungekuwa ukombozi wa mwanzo wa kuanza kuyaona matunda ya ule ugunduzi, bahati mbaya hali ilivyo ni kama vile hili jambo linasuasua sana na linawezekana kabisa sijui lisiwezekane linatupa tabu. Kwa sababu leo makampuni yote matano ambayo ndio yangeshirikiana katika ujenzi kinu hiki, ukichukua British gas, orfil energy, start oil, Exon Mobil na hata Petrobrass tulidhani ofisi zao zingekuwepo Lindi na Mtwara na ziwe active, tulidhani vifaa vyao mahelkopta yao yale, meli zao zile leo hazionekani? (Makofi)

Sasa tunataka Serikali ituambie kinachoendelea ni nini huu mradi bado upo? Ukisoma kwenye hotuba ya Nishati na Madini unaona imezungumzwa ka-para kamoja lakini kweli mradi mkubwa wa zaidi ya dola bilioni 33 kitu unazungumzwa kwa para ndogo kama vile hakuna kinachoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani Serikali hapa kuweni serious tuambieni ukweli huu mradi upo au haupo?

Na kama haupo tujue namna ya kufanya na kama upo unaanza lini tulijua mwanzoni tatizo lilikuwa ni ardhi. Rais amefuta hati hili jambo lilitakiwa liwe limekwisha kwanini bado inaendelea hivi na ziko habari kwamba hawa jamaa sasa wanahamia Msumbiji, tuambieni ukweli hali ikoje, mradi upo au haupo? Na tungedhani kwa sababu mradi huu ungeanza uchumi wa Lindi ungebadilika, pesa zingeingia nyingi hata katika ile process yenyewe tu ya kuujenga huu mradi ambao ungechukua zaidi ya miaka nane, lakini zaidi ya dola bilioni nne zingiingia Lindi zingebadilisha maisha ya watu wetu pale. Lakini kwa hali tunavyoenda nayo tunapata mashaka. Sasa ni vizuri Serikali tukawa wa kweli, kauli ya Serikali itolewe katika jambo hili, tukowapi, tunaenda wapi, nini matumaini ya mradi huu mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo nilitaka nilizungumzie la mwisho nadhani kwenye hotuba yako Mheshimiwa Waziri pamoja na uzuri wa hotuba hii, lakini kuna mahali umezungumzia sera za mapato. Hapa ukisoma umeweka mipango karibu saba, lakini Mheshimiwa Waziri mipango yote inalenga kubana na kukamua wakwepa kodi na kukamua ukusanyaji wa kodi. Sijaona mpango straight unaozungumza namna ya ku-stimulate growth ya economy ya nchi yetu. Sasa kama hata…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)