Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi za Ubaharia wa Shirika la Kazi Duniani na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Vitambulisho vya Mabaharia Na. 185 wa Mwaka 2003 wa Shirika la Kazi Duniani

Hon. Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi za Ubaharia wa Shirika la Kazi Duniani na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Vitambulisho vya Mabaharia Na. 185 wa Mwaka 2003 wa Shirika la Kazi Duniani

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii nichangie Azimio la Kuridhia Mkataba wa Mabaharia nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda niipongeze Serikali kuleta hili Azimio kwa sababu limekuja wakati muafaka, tumekuwa tukiona vijana wa Kitanzania wamekuwa wakipata shida huko nchi za nje wanapokwenda kufanya kazi za ubaharia. Pia wamekuwa wakipoteza mali zao kwa sababu Tanzania ilikuwa haijaridhia hii mikataba ambayo ni mikataba takribani 37 ambayo Tanzania ilishindwa kuridhia kwa muda wa miaka hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuunganisha Mikataba hii 37 kuleta mkataba huu itawawezesha vijana wetu wa Kitanzania kupata ajira kirahisi kwenye meli za nje, itawezesha pia Tanzania nchi yetu kusaidia kwenye ajira za kazi kwa



sababu tuna ukosefu wa ajira vijana wetu wataweza kuajiriwa nje na Serikali itaweza kupata manufaa zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninalo angalizo dogo kuhusu sheria ambazo zitatumika kwa sasa hivi tunazo sheria za SUMATRA, pia tunazo sheria za Zanzibar kwa sababu tunakwenda kuingia Mkataba wa Kimataifa itabidi Serikali ilete hizi sheria izirekebishe maana yake flag country itakuwa ni moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Zanzibar wanasajili meli wanaye Agent anayesajili hizi meli kule Dubai, lakini SUMATRA hawana. Ningeomba Serikali ijaribu kuliangalia hili suala kwa sababu mkataba huu hautaonesha kwamba hii meli imesajiliwa na Zanzibar na hii imesajiliwa Tanzania Bara, inabidi sheria hizi ziunganishwe kwa pamoja za ZMA na SUMATRA kwa sababu mkataba ni wa Kimataifa, kitakachokuwa kinaeleweka hapa ni sovereignity of the state ambayo ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Haitakuwa busara kwamba sasa hivi hii meli imesajiliwa na Zanzibar, kwa hiyo ikipata pale matatizo tutasema kwamba hii meli ilisajiliwa na ZMA au hii ilisajiliwa Tanzania Bara, ningeomba uoanisho wa hizi sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono Azimio hili.