Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi za Ubaharia wa Shirika la Kazi Duniani na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Vitambulisho vya Mabaharia Na. 185 wa Mwaka 2003 wa Shirika la Kazi Duniani

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi za Ubaharia wa Shirika la Kazi Duniani na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Vitambulisho vya Mabaharia Na. 185 wa Mwaka 2003 wa Shirika la Kazi Duniani

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata muda huu wa kuchangia kwenye mawasilisho haya. Kwanza nipongeze kuletwa huu Mkataba ambao utaweza kusaidia kurekebisha kasoro nyingi zinazotokea kwenye sekta hii ya marine.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kujielekeza hasa kwenye mambo machache kwa sababu ya muda, hasa suala zima la Mabaharia ambao wanasafiri na vyombo ambavyo vya kuchukulia hasa mizigo kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara na vile vingine vinaenda Mafia na vingine vinaenda mpaka Mtwara.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mabaharia hawa hawana mikataba rasmi, lakini vyombo vile vinakaguliwa na SUMATRA, vinapewa leseni ya kusafirisha mizigo, lakini uhalali wa ufanyajikazi wao katika zile meli haupo. Mtu unaweza kuingia leo kazini kesho ukasimamishwa, ukakoseshwa mshahara na mambo mengine ambayo hayastahiki kufanyiwa wafanyakazi hasa wa meli.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile suala zima la vyombo ambavyo vinasafirisha abiria hasa katika bandari zile ndogo ndogo mfano Mkokotoni kuja Tanga, Kipumbwi nao vilevile wale Mabaharia wanaofanya kazi ndani ya vyombo vile zile fiber, boti ndogo ndogo hakuna mikataba ya ufanyaji kazi katika meli zile au boti zile ambazo zinakwenda katika maeneo yale. Linapotokezea lolote Baharia yule anakuwa hatambuliki, anayetambulika pale ni mwenye chombo au Nahodha kwa kiasi kidogo sana. Naomba vilevile hili Waziri aje atupe maelezo hatua gani SUMATRA itazichukua kudhibiti hali hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine kwenye hili ni suala zima la wanafunzi ambao wanasoma katika Chuo cha Marine kile kilichopo Dar es Salaam, wanafunzi wale wanapata nafasi ya kwenda kufanya kazi katika meli za nje, lakini ikifika muda kutaka kuja ku-renew zile leseni zao, pale kwenye kile chuo wanatakiwa wasome tena...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.