Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Stephen Julius Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. STEPHEN J. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii ya kuchangia hoja hii iliyopo mbele yetu.

Mheshimiwa mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuunga mkono hoja hii na nizungumze mambo mawili. Kwanza ni kwenye eneo la utafiti, lakini la pili ni kwenye usimamizi na utekelezaji wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, itifaki hii ni muhimu sana kwa Taifa letu na itaweka ulinzi wa rasilimali zetu hasa za baharini na tafiti zinazoendelea kufanyika zinaonesha kwamba kwenye bahari zetu tuna rasilimali zenye thamani kubwa sana inawezekana kuzidi rasilimali zilizopo nchi kavu. Kwa hiyo, ushauri wangu kwa Serikali ni kuongeza uwezo wa vyombo vyetu vya utafiti hasa kupitia vyuo vikuu vyetu ili tuwe na uwezo mkubwa wa kibajeti na kitaalam na sisi tuweze kufanya tafiti hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kushirikiana na vyombo vya utafiti va Kimataifa ili kujua kinachoendelea kwenye tafiti ambazo zinafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo tafiti nyingi zinaendelea hapa nchini wakati mwingine unaweza kukuta hata kwenye Wizara Serikali haitambui kama tafiti hizi zinafanyika. Kwa mfano, kuna taifiti moja inafanyika na Chuo Kikuu cha Florida cha Marekani wa kutafiti maji ya mito yetu kwa mfano Mto Wami, Mto Mara, Mto Morogoro na Mito mingine miwili hapa Tanzania lakini unakuta wale wanaotafiti hawana coordination kabisa na Serikali, kwa hiyo mimi ombi langu kwa Serikali kwamba baada ya kupitisha ikawa sheria basi tusimamie na tuhakikishe tunasimamia na tunashiriki katika tafiti zinazofanywa ndani na Mashirika ama makampuni ya Kimataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutimize wajibu wetu kama Wabunge wa kutunga Sheria na Serikali itimize wajibu wake wa kutekeleza haya ambayo tunayapitisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru, naunga mkono hoja.