Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii na mimi nichangie kwenye itifaki hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema naiunga mkono itifaki hii kwa sababu inazungumzia maisha ya sisi watu wa Pwani na sisi watu wa Pwani bila bahari maisha hayapo. Vilevile niseme kwamba itifaki hii itakuwa na maana tu kama itatuhakikishia watu wa Pwani maisha yetu yataboreka. Kama itifaki hii haitatusaidia maisha yetu kuboreka haina maana, kama itifaki hii haitatuhakikishia kuboreka kwa maisha ya watu wa Pwani basi itifaki hii haina maana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema haya kwa sababu mwaka 1996 tulisaini mkataba ule uliokuwa unazungumzia udhibiti wa bahari ukanda wa Afrika Mashariki. Mwaka 2010 tukaiboresha itifaki ile tukasaini. Nataka tu nijiulize hivi tangu 1996 tuliposaini watu wa Pwani maisha yamekuwa bora? Nini kinatuhakikishia leo kwa kusaini itifaki hii kwamba maisha ya Pwani yataboreka? Utafiti umetuonyesha kwamba itifaki hii katika utekelezaji wake tangu mwaka 1996 umekuwa na changamoto kubwa ya kimfumo wa usimamizi wa taasisi za usimamizi, vilevile changamoto kubwa ya kifedha. Tafiti hazifanyiki na zikifanyika zinafanyika kwa ufinyu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka leo watu wa Pwani zana tunazotumia kwenye uvuvi ni zana duni, tumekuwa tukitamani tuyaone yanayofanyika kwenye sekta ya kilimo kupewa pembejeo na vitu vya namna hii, yafanywe kwenye sekta ya uvuvi hayafanyiki. Tumekuwa tukitamani tuyaone yanayofanyika kwenye sekta ya mifugo kwa watu wa sekta ya uvuvi hayafanyiki. Ndiyo maana mnashuhudia watu wale wanaendelea kutumia zana duni za tangu enzi ya Nabii Nuhu. Ndiyo maana mnashuhudia uvuvi wa kutumia mabomu unaendelea, ndiyo maana mnaona mazalia ya samaki yanaendelea kuharibika kwa sababu tumeitupa mkono sekta ya uvuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifurahi kwenye Ilani yetu tuliposema kwamba katika kipindi hiki tutaleta meli tano za uvuvi. Nataka tu niikumbushe Serikali yangu, mwaka wa pili huu sasa wa utekelezaji, tumebakia na miaka mitatu tujitahidi ahadi ile itimie. Lakini hata ahadi hiyo ikitimia bado asilimia kubwa ya wavuvi watakuwa hawana zana za kisasa kwenda kuvua, ndiyo maana leo unaona hata kwenye uuzaji wetu wa samaki tunategemea sana samaki wa kutoka Ziwa Victoria, uvuvi kwenye eneo la baharini uko duni. Twendeni tukawekeze kwenye blue economy, twendeni tukahakikishe ufugaji wa samaki unafanyika kwenye ukanda wa Pwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jarida la Sofia la FAO linatuambia hivi takribani watu milioni 57 wana… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.