Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mungu kwa kunijalia afya na nguvu za kuendelea kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kyerwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kipekee kuipongeza Serikali yangu kwa kazi nzuri inayofanyika kuanzia Rais wetu, Waziri Mkuu na Serikali kwa ujumla. Nampongeza sana Waziri wa Maji, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii muhimu sana kwa Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la maji ni kubwa sana kwa Taifa letu, maeneo mengi hawana maji safi na salama, pia hata wale wanaopata maji wanayapata kwa umbali mrefu sana zaidi ya kilometa kumi mpaka 20. Kitu ambacho kinarudisha nyuma shughuli za maendeleo na kushusha uchumi wa Taifa na katika hili waathirika wakubwa ni wale walio vijijini ambao ni wakulima zaidi ya asilimia 70 na ndiyo wazalishaji wakubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe sana Wizara ikiwezekana iongeze pesa kwenye bajeti kwa sababu bajeti hii imeshuka sana kulingana na mahitaji ni makubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Jimbo langu hali ni mbaya sana ya upatikanaji wa maji safi na salama, niishukuru sana Serikali kwa miradi ya zamani ya miaka ya 1970 ambayo ilikuwa imechakaa sana. Kazi ya kuboresha miundombinu imeanza katika kata ya Mabila, mradi wa Kilela - Isingiro, Kagenyi, Lukurayo na miradi mingine midogo. Miradi hii ni sehemu ndogo sana ya mahitaji ambayo ikikamilika itasaidia kama asilimia 15.

Mheshimiwa Naibu Spika, suluhisho la kuwapatia wananchi wa Kyerwa maji, niendelee kushukuru Serikali kwa mradi mkubwa wa vijiji 57 kwenye kata 15 ambao uko kwenye hatua ya usanifu ambao hatua hii itakamilika mwezi wa Septemba, 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulileta mapendekezo kuomba shilingi bilioni 12 kama kianzio ili tunapomaliza usanifu kazi ianze kuwanusuru wananchi wa Kyerwa na tatizo la upatikanji wa maji safi na salama, pia kuwandolea wananchi usumbufu wa kufuata maji mbali zaidi ya kilometa 20.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasikitika sana kuona kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018 mapendekezo yetu hayajakubalika kitu ambacho kitasababisha kusubiri mwaka 2018/2019. Naiomba sana Wizara, niko chini ya miguu yenu na kwa unyenyekevu mkubwa nakuomba Mheshimiwa Waziri uangalie namna yoyote ya kupata pesa ili tunapomaliza usanifu kazi ianze haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama walivyoshauri Waheshimiwa Wabunge wenzangu kuongeza shilingi 100 kwenye mafuta na mimi nashauri Serikali yetu ikubali ili kuwaokoa Watanzania wanaopata mateso makubwa ya ukosefu wa maji safi na salama. Pia umbali wanaoupata kufuata maji mbali na baada ya kukubali ombi hilo na Kyerwa maombi yetu yapokelewe ya kutengewa shilingi bilioni 12 ili kuanza mradi wetu mkubwa wa vijiji vyetu 57 na kata 15, naomba sana Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na maombi hayo bado kuna kata zingine ambazo hazijafikiwa na mradi mkubwa wa vijiji 57, niendelee kuiomba Serikali kututengea pesa ili kuwapatia huduma hii muhimu wapiga kura wangu. Najua Serikgu yatazingatiwa na kupewa umuhimu sana.

Mhesali yangu na Mheshimiwa Waziri wangu ni sikivu, maombi yanhimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nashukuru na naunga mkono hoja.