Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Naibu Spika, hongera sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kuandaa vizuri hotuba ya Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepitia majedwali katika kitabu cha hotuba jedwali namba 13 la orodha ya visima vilivyochimbwa hadi mwezi Machi, 2017, sehemu inayoonesha uwezo wa kisima kuna maeneo yameachwa wazi na maeneo mengine yameachwa wazi kwa uzembe. Kwa mfano, kisima namba 204 cha Msijute kilichofadhiliwa na ESRF na kuchimbwa na Wakala wa Visima wa Serikali kuna uzembe mkubwa umefanyika. Baada ya kuchimba kisima waliletwa watu wa kupima uwezo wake wakatoa taarifa kwamba hakuna maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wa ESRF wamehitaji wapate taarifa itakayowaelekeza nini kifanyike ili maji yapatikane lakini miezi imepita bila mafanikio, binafsi wakala waliniambia niongeze shilingi milioni tatu ili wachimbe kisima kingine na baadae mwezi wa nne nikaambiwa niongeze shilingi milioni sita ili nichimbiwe kisima kingine. Ajabu ni kwamba watu wa bonde walipokuja wamepima na kuona kwamba maji yapo kwa asilimia 30 ya mita 150 zilizochimba, wamesema kwamba wale waliojaribu kupima uwezo wa kisima walitumia pump kubwa ambayo ilikausha maji kwa muda mfupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mapendekezo yao ni kwamba zingetumika pump zenye uwezo tofauti na pia ilibidi wa-flash kisima, ushauri wangu kisima kile ni kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Msijute ambao walimuamini Wakala wa Visima wa Serikali. Ni vema iandikwe taarifa ya ukweli na uwazi kwa ESRF ili aweze kuchukua hatua za ziada kuwasaidia wananchi wa kijiji cha Msijute wapate maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, chunguzeni visima vyote ambavyo havioneshi uwezo wake mjue sababu na taarifa itolewe kuepusha ubabaishaji wa baadhi ya wachimbaji visima. Fikeni katika maeneo husika mkutane na wachimbaji na Mamlaka za Mabonde na wafadhili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.