Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na naomba kuongeza michango yangu baada ya kuchangia kwa kuongea.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo linalosumbua katika miradi ya maji inayoendelea kwani imeshindwa kukamilika, miradi ya maji inayoendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba ni minne, hali ya ujenzi hadi sasa ni kama ifuatavyo:-

(i) Isunga hadi Kadashi asilimia 50, kazi kubwa iliyobaki ni ulazaji wa bomba ambapo bomba linalohitajika ni kilometa 22.

(ii) Igunguya hadi Nyanhiga mpaka Igunguya asilimia 95, mradi upo katika majaribio na Nyanhiga amebakiza kulaza bomba kilometa 11.

(iii) Igumangobo asilimia asilimia 75, amebakiza kulaza bomba mita 150 na kukamilisha ujenzi wa tenki.

(iv) Mhande hadi Shirima mpaka Izizimba ‘A’ asilimia 45 kazi kubwa iliyobaki kutandaza bomba kuu kilometa 40 na mtandao wa bomba vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, sababu kubwa ni kuwa wakandarasi kutoiamini Serikali kuhusiana na malipo yao kutokana na ucheleweshaji uliojitokeza huko nyuma. Serikali inasema nini katika kujenga imani kwa Wakandarasi ili waweze kufanya kazi kwa haraka na wakandarasi kushindwa kujituma au kuwa wazalendo kwa kufanya kazi kwa kasi na kwa ubora tarajiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba visima vingapi ni vibovu na viko maeneo gani na sababu ya ubovu, tuna visima 188 vibovu na sababu ya ubovu kunaibiwa kwa pampu, kuharibika kutokana na umri mkubwa na kuishiwa maji kutokana na mabadiliko ya tabianchi kutokana na Sera ya Maji ya mwaka 2002, uendeshaji na matengenezo kwa maji vijijini asilimia 100 ni wananchi kupitia Jumuiya za Watumiaji Maji (COWSO) wakati kwa Mamlaka za Maji za Wilaya na Mikoa Serikali inasaidia kutoa ruzuku.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali haioni imefika wakati Kamati za Maji au Jumuiya za Maji Vijijini kusaidiwa hasa kwa kukarabati visima vilivyopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, visima hivi vibovu viko katika maeneo yafuatayo; Bungulwa (5), Bupamwa (3), Fukalo (4), Hungumalwa (4), Malya (12), Mantare (8), Bungando (2),
Igongwa (4), Ilula (4), Iseni (1), Kikubiji (5), Maligisu (3), Malya
(13), Mhande (5), Mwabomba (9), Mwagi (7), Mwakilyambiti(
7), Ng’hundi (6), Ngudu (6), Nkalalo (2), Nyambiti (11), Sumve
(17) na Walla (18).

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kata ambazo hazina kabisa huduma ya maji safi na salama ni kata ya Shilembo ambapo kuna kisima kimoja tu vijiji vyote, vijiji ambavyo havina kabisa huduma ya maji ni Mantare (Mwampuru) na Ngulla (Nyambuyi).

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.