Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kushauri yafuatayo; Serikali iongeze bajeti kwenye fungu la maendeleo na pesa hii ipo kwenye mafuta, umeme na maji yenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mingi ya umwagiliaji inakumbana na pingamizi kwa kuwa ujenzi wa miundombinu umejielekeza kujenga mabwawa kukinga maji. Hapa wananchi wanaogopa kupoteza ardhi zao, kwa nini tusitumie mfumo wa visima virefu na wind wheels kuweka maji kwenye matanki na kusambaza kwa gravity kwa kuwa gharama ni nafuu na eneo linalopotea ni dogo. Mradi kama huu upo kata ya Kanyalla Ibada na umepingwa na wananchi kwa sababu hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tatizo la maji Mjini Geita, hivi sasa Mradi wa Maji wa LV-Watsan unasuasua sana mpaka leo miezi minne imepita, mkandarasi ameshindwa kumaliza kazi, nashauri mtu huyu afutwe kwenye orodha ya wakandarasi kwa kuwa hana uwezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uhaba wa maji katika Mji wa Kasamwe, naishauri Serikali kuunganisha mradi mpya wa maji wa fedha za India kwa Mji wa Geita ili maji yake yafike Kasamwa, kwa sababu kwa mujibu wa wataalamu hivi sasa kuna tanki kubwa la maji Buhalanda ambalo lipo kilometa 10 tu kutoka Kasamwa na ambapo maji yatafika kwa gravity na kwa kuanzia ziwekwe DP’s tu kwenye mitaa ili wananchi wapate maji, badala ya sasa kutumia bwawa ambalo gharama yake ni kubwa

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali kunipa majibu maji katika Kata za Shiloleli, Bulela, Ihanamilo, Nyanguku, Mgusu na Bung’wangoko yatafika kupitia mradi huu wa fedha za India? Kwa sababu hizi kata ni sehemu ya kata za Mji wa Geita Jimbo la Geita.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.