Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya kwa kutatua changamoto ya maji. Nimpongeze Waziri na watumishi wa Wizara wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali iweze kutazama upya upande wa tozo ya mafuta kuweka shilingi 100 ili Watanzania waweze kupata maji kwa kutumia mfuko katika fedha za maji zilizopelekwa hadi Machi kati ya shilingi 181,209,813,609. Utaona asilimia ni 52.7 ambazo ndizo zilizotokana na tozo hiyo, upo umuhimu mkubwa kuhakikisha kuwa pesa hiyo ndiyo inafanya kazi kubwa.

Mheshimiwa Mwenyikiti, ninaishukuru Serikali kwa kutupatia pesa kwa ajili ujenzi wa bwawa la Itabi, Wilaya yangu ya Itilima pamoja na kupata pesa za Halmashauri kuingia katika utekelezaji wa visima kumi na kupata shilingi milioni 49 kuweka pump kwenye mabomba pamoja na kupata fedha za mradi wa mabwawa sita ya Mwamapalala, Nhobora, Rugulu Sunzura, Chinamili na Sawinda yote hii ni juhudi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa mipango yote hiyo iliyoanzishwa kwenye bajeti na kiwango cha pesa kilichopangwa na Serikali ifanye utaratibu mzuri wa upatikanaji wa fedha hiyo katika Wilaya ya Itilima.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.