Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. KAPT. (MST). GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji wa maji mradi wa maji Makonde hauridhishi. Tunapata maji ya bomba chini ya asilimia 30 ambayo ni kidogo sana ukilinganisha kitaifa. Moja, booster station ya kati ya Mkunya na Makote ilijengwa tangu 2006 lakini haijakamilika na haijakabidhiwa, kwa nini hawaifanyii kazi? Serikali ieleze mradi huu utakamilika na kukabidhiwa lini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mbili, mabomba na mitambo ya Mradi wa Maji Makonde yamechakaa. Chanzo cha Mkunya kinatakiwa kuwa na pump tatu lakini iko moja tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, chanzo cha Mitema kinahitaji pump sita ila ziko mbili tu. Mradi uliagizwa kutangaza tenda ya kubadilisha mabomba kwa shilingi bilioni mbili, mkandarasi alipatikana lakini fedha hazikutumwa. Serikali inunue kwanza pump na iharakishe upatikanaji wa mkopo kutoka India, ulioahidiwa, ili mradi uweze kukarabatiwa na kuongeza upatikanaji wa maji. Msimu wa mvua kwetu umekwisha wasio na visima hawawezi tena kukinga maji ya mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, skimu ya umwagiliaji ya Chikwedu – Chipamanda. Tumeelezwa mkataba bado kwa sababu taratibu za manunuzi zimechelewa Ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya. Hili halikubaliki, halmashauri isimamiwe skimu iweze kukamilishwa tuweze kuendeleza kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nne, Wilaya ya Newala ilikuwa na mradi mdogo wa maji – Luchemo. Mradi huu ulikumbwa na mafuriko mwaka 1990 hivyo ukafa. Wizara haijachukua hatua za kuufufua. Nashauri mradi huu ujengwe upya maana wananchi waliokuwa wanategemea mradi huo sasa hawapati maji safi ya bomba.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.