Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kuwapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kujitahidi kwa dhati kabisa katika kuhakikisha kuwa suala la maji linatimia kwa nguvu zote, ukizingatia kwamba maji ni uhai.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na changamoto zilizopo napenda kuishukuru Wizara kwa kututengea fedha kwenye mradi wa HTM ambao kwa muda mrefu ulitakiwa uwe umeshakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alitembelea Jimboni kwetu na kuahidi kwamba tukiwa tunasubiri mradi mkubwa kutoka kwenye ufadhili wa India, basi Serikali itatoa shilingi bilioni mbili ili kukarabati mradi wa HTM uliopo sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Engineers wamekuja na wameshafanya kazi zote za michoro ya ukarabati wa HTM na wameshakabidhi Wizarani. Basi naomba utekelezaji ufanyike kama ahadi ya Mheshimiwa Naibu Waziri alivyowaahidi wakazi wa Handeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri kwenye majumuisho yake atufafanulie ni lini mradi huu mdogo unaanza, wakati tukiwa tunasubiri ule mkubwa? Ahsante.