Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupata ufafanuzi wa vigezo vinavyotumika kugawa fedha za Miradi ya Maendeleo ya Maji Vijijini. Kwa mfano katika ukusara wa 140 jedwali 5(a) Monduli imetengewa shilingi 646,914,000. Jambo ambalo ni kinyume kabisa na matarajio ya mapendekezo ya bajeti ambayo ilikuwa bilioni nne. Ni namna gani tutatekeleza miradi ya wananchi kwa kiasi hiki kidogo?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali itusaidie kuimarisha chanzo cha maji Ngaramtoni (kisima) ili kukidhi uhitaji wa maji ambapo kwa sasa miradi mingine imeanzishwa kwa kutumia kisima cha awali. Serikali haijapanga fedha miradi ya vijiji viwili; sehemu ya vijiji kumi ambavyo vilikuwa vimebaki awamu ya pili.