Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, bili ya maji. Kuna malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba bili za maji ni tofauti na ilivyokuwa awali, pia hata kusoma wanakuwa wanakadiria tu na kupelekea kuleta hali ya sintofahamu kwenye Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mita za maji kuchezewa. Suala hili limekuwa ni tatizo na mambo haya yanafanywa na watumishi wenyewe wa Idara ya Maji au watu wanaokuwa wafanyakazi wa Ofisi za Idara ya Maji kwenye Halmashauri zetu na mikoa yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, uharibifu wa vyanzo vya maji. Elimu inatakiwa kutolewa kwa wananchi wetu ili wajue athari za kuharibu vyanzo vya maji kwani hatuwezi kukomesha tatizo hilo bila kutoa elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu ya maji ni mibaya. Suala hili linahitaji Wizara tatu kukaa kwa pamoja ili kuimarisha tatizo la maji katika Halmashauri zetu. Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Miundombinu.

Mheshimiwa Naibu Spika, elimu ya uvunaji maji ya mvua. Kumekuwa na matatizo sugu ya ukosefu wa maji katika Mkoa wa Rukwa wakati mvua zimenyesha na kusababisha mafuriko na kuua watu na maafa. Kwa nini Serikali isiwe na utaratibu wa kuhifadhi maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Kilimo, Mifugo na uvuvi na Wizara ya Maji na Umwagiliaji kukaa pamoja na kupanga utaratibu wa kutoa elimu kwa wananchi wanaozunguka vyanzo vya maji kulima mazao ambayo hayataathiri vyanzi vya maji na pia kutowaathiri wananchi kupata njaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, watumishi wa Idara ya Maji wasio waaminifu wamepelekea malalamiko makubwa kwa wananchi kwa kuwapa vifaa vibovu au kuchezea mita na kusababisha bili zisizo na uwiano.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji na Umwagiliaji itengeneze mita kama ilivyo LUKU za umeme ili kuondoa malalamiko kwani kila mtu au mteja anajua amelipa kiasi gani na ametumia kiasi gani kumaliza kabisa malalamiko.

Mheshimiwa Naibu Spika, elimu. Ili kulinda vyanzo vya maji, wananchi wakielimishwa vizuri juu ya kulinda vyanzo vya maji matatizo mengi yataisha au kupungua kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pesa iliyotengwa ni ndogo iongezwe kulingana na umuhimu wa maji katika maeneo mengi nchini. Pesa iliyotengwa haiwezi kumaliza tatizo la maji nchini. Nashauri Serikali iongeze pesa.