Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Naomba kupongeza kazi nzuri zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano na Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Nkasi Kusini tuna miradi ya maji inayoendelea. Miradi hiyo imekuwa ya muda mrefu na imeacha matumaini yakipotea kwa wananchi. Naomba Serikali iione miradi hii kwa namna ya pekee na ilete tija kwa wananchi wake. Naitaja kama ifuatavyo:-

Mradi wa Maji wa Bwawa la Kawa ni wa muda mrefu, umetumia fedha zaidi ya bilioni mbili, wananchi bado hawajaanza kupata maji katika Vijiji vya Frengelezya, Nkuudi na Kalundi. Pia natoa mapendekezo kuwa, mradi huu utakapokamilishwa upeleke maji Sekondari ya Kipande na Kijiji cha Myula.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa kutoka Kate Milimani kwenda Vijiji vya Nkata, Ntemba, Kitosi, Ntuchil, Ifundwa, Msilihofu na Isale ni mradi muhimu, uanze mara moja. Najua kwa sasa mtaalam mshauri yuko site, tuna fedha kwenye bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji King’ombe. Mradi una upungufu kwenye njia zake, mradi una mabomba yako nje nje, dosari zirekebishwe na naomba ukamilike na nashauri wananchi waulinde mradi wao. Nitamshambulia sana mtu anayehujumu njia ya maji, gharama ya mradi ni kubwa, zaidi ya milioni 720.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Kijiji cha Mpasa naomba uanze kutekelezwa. Wananchi wanasubiri kwa muda mrefu na imani inawatoka sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Chala Mji Mdogo. Nimeona Wizara imetenga bilioni mbili kwa ajili ya upembuzi wa kina kushughulikia miji kadhaa ukiwepo wa Chala.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba fedha hii iongezwe, sidhani kama inatosha. Angalia Ukurasa wa 164(31) wa Hotuba. Mji wa Chala una shida ya maji kwa kiwango cha juu sana na mamlaka yake imeanza haina mapato yoyote kwa kuwa hakuna maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Kisura (Kijiji). Kazi inaendelea vizuri kwa sasa, japokuwa ilichelewa sana. Kasi hii iendelee hadi mwisho wa mradi, wananchi wanapata shida.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi la Kutafiti Maji kwenye Vijiji vya Kasu, Katani, Milundikwa na Kantawa. Vijiji hivi havina maji ya uhakika, naomba Serikali ifanye kazi ya kutafiti ili kusaidia vijiji vyote na Sekondari za Kasu na Kambi ya Jeshi, pia Milundikwa. Naomba vilevile Kata za Wampembe, Ninde na Kizumbi wafanyiwe utafiti maji ya mseleleko yanaweza kupatikana.