Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mlimba lenye vijiji 61 na kata 16 maji tunayapata wakati wa mvua (masika) na yakija yanaharibu makazi, barabara, mashamba na kadhalika. Kuhusu maji safi na salama, wananchi wa Jimbo la Mlimba kwao ni tabu sana.
Mfano, katika Mji Mdogo wa Mlimba, Kata ya Mlimba kuna kisima kimoja ambapo maji yanapatikana kwa mzunguko wa wiki mara moja tu. Kata nyingine 15 na kwenye shule za sekondari, za msingi na kwenye zahanati hakuna maji kabisa. Hivyo, naomba Mheshimiwa Waziri/Naibu Waziri aje Mlimba ili ajionee mwenyewe hali ilivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma kwenye Taarifa/ Hotuba ya Mheshimiwa Waziri kuhusu mradi wa mfereji wa umwagiliaji Kijiji cha Njage kuwa mradi huo unaleta tija. Ukweli ni kwamba mradi huo hauna faida wala tija kwa wananchi kwani, ingawa ni umwagiliaji mfereji huo hauna maji wakati wa kiangazi, bali wakulima hulima wakati wa masika tu, hivyo hulima kwa mwaka mara moja tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Waheshimiwa Mawaziri waje Jimbo la Mlimba washuhudie miradi iliyopo huko ambayo haina mwendelezo. Napendekeza pesa ikusanywe kwa kuweka tozo kwenye sigara, maji ya chupa, soda, bia, ili ziingie kwenye Mfuko wa Maji na fedha hizo mjini zipelekwe asilimia 30 na vijijini asilimia 70.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.