Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali iliyo chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Busokelo ni jimbo changa na miundombinu ya maji ni tatizo kubwa sana, hasa Mji wa Lwangwa, Kandate, Ntaba na maeneo mengine. Miradi wa Masoko na Mwakaleli I na II ni miradi ya miaka mingi sana lakini hadi sasa haijakamilika. Kwa sababu hiyo, naomba Serikali iweze kutimiza ahadi ya viongozi wetu wa Serikali. Naomba majibu ya Serikali, ni lini Miradi ya Masoko, Mwakaleli I na II itakamilika?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.