Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naunga mkono hoja ya bajeti ya Wizara hii. Pamoja na hayo pia nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuweka kipaumbele cha maji kwa kuzingatia pia kuwa ipo katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Maji, Mheshimiwa Injinia Lwenge, Naibu Waziri wake, Mheshimiwa Injinia Kamwelwe pamoja na timu nzima ya Wizara hiyo kwa uzinduzi wa miradi mikubwa ya maji ya Ziwa Viktoria na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo yote, maji ni uhai, bila maji hakuna maisha. Huduma ya maji mijini imekuwa ni tatizo. Kwa mfano, kule Jijini Mbeya maji hukatika mara kwa mara na kuletewa bili kubwa ya maji na nina uhakika hili ni tatizo katika miji mingi tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa 71, unazungumzia kuhusu uboreshaji huduma ya maji katika Jiji la Dar es Salaam, hili limekuwa ni tatizo la muda mrefu. Kwanza sewage system yake ni mbovu sana katika jiji lote hususan mvua ikinyesha na hivyo kusababisha uharibifu wa mazingira na magonjwa ya mlipuko. Katika eneo la Mbezi Beach Juu kuelekea Hospitali ya Masana–Goba Road, maji yamekuwa hakuna kwa miaka mingi na hakuna dalili ya ufumbuzi wa tatizo hili, zaidi tu ya wananchi kupigwa danadana kuwa kuna bomba la mradi wa Wachina. Wananchi wamekuwa wakinunua maji kwa gharama kubwa kwa miaka mingi sana bila suluhisho wala ufumbuzi wowote.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mbeya Jiji kulikuwa na mradi mkubwa sana uliozinduliwa kwa msaada wa Serikali ya Ujerumani (KFW) lakini hadi leo maji yanakatika hovyo na bila taarifa yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, nahitaji kujua Serikali ina mkakati gani katika suala zima la Mfuko wa Maji. Mfuko huu utasaidia sana kutatua kero nyingi zisizo za lazima kimkakati mijini na vijijini. Mfuko huu unatakiwa uwe mkubwa kibajeti ili kuboresha huduma ya maji nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.