Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata fursa ya kuchangia kwa maandishi kuhusu Wizara hii. Kwa masikitiko makubwa nalaani kitendo cha kutokuwa na uhuru wa tasnia ya habari kama inavyotekelezwa na Bunge lako Tukufu. Kwa sisi akinamama na vijana katika nchi hii tumekuwa tukipambana na maisha na mara nyingi tulikuwa tunasahaulika. Uhuru wa vyombo vya habari ulifanya wanawake wengi waingie kwenye tasnia ya siasa kwa kuwa wamekuwa wakiwaona wenzao waliotangulia wakifanya uwakilishi wao Bungeni vizuri na hii ilihamasisha wanawake wengi kuona kuwa wanaweza.
Mheshimiwa Spika, akina Getrude Mongela, Asha Rose Migiro, Spika aliyestaafu Mheshimiwa Anne Semamba Makinda, Mheshimiwa Halima Mdee, Mheshimiwa Pauline Gekul na wengine walionesha mfano kuwa wanawake tunaweza. Kwa namna hii inaonesha kuwa, Bunge hili linataka kudidimiza kufikisha 50 kwa 50 kwani wengi wanawake waliogombea wameweza kushinda Ubunge wa Majimbo na waliaminiwa na wananchi wao kwa kuwa walionekana wakitetea maslahi ya Watanzania.
Mheshimiwa Spika, nashauri Bunge hili lirushwe live ili wanawake tupate fursa ya kuonekana ili kuondokana na kuwa Wabunge wa Viti Maalum.
Mheshimiwa Spika, suala la Zanzibar. Nchi yenye utawala bora haina woga wowote, lakini nchi yetu imeonesha ufinyu wa demokrasia kwa suala la uchaguzi wa Zanzibar. Serikali inapaswa kutumia busara zaidi na si ushabiki kuhakikisha Zanzibar inakuwa tulivu.
Mheshimiwa Spika, kuhusu Watumishi hewa; naunga mkono hotuba ya (KRUB) iliyofafanua jinsi udhibiti wa wafanyakazi utakavyokuwa kwa kuunganisha mfumo, mfano, mfumo wa Utumishi wa Umma uunganishwe na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kama vile NSSF, PSPF, LAPF, GEPF na kadhalika. Kwa wale wahusika wote pia wachukuliwe hatua za kisheria.
Mheshimiwa Spika, nimeshukuru na naunga mkono hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni (KRUB).