Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe maoni yangu kwa maandishi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 72 unataja miradi ya visima katika Kata za Gongolamboto, Chanika, Pugu Mpera, Kitunda na Ukonga. Kata hizi pia zilitajwa mwaka wa fedha 2016/2017 na hadi sasa visima hivyo havijakamilika. Naomba kujua ukweli wa miradi hii kama kweli ipo. Nashukuru Waziri na Naibu wake kwa ushirikiano wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 73 ametaja miradi tarajiwa katika Kata za Msongola, Chanika, Gongolamboto, Pugu na Kitunda. Kata hizi nazo zimekuwa zikitajwa kila mwaka bila mafanikio. Kwa uhakika kuna shida kubwa ya maji katika Jimbo la Ukonga na hasa kwenye maeneo ya huduma za umma kama shule, zahanati, Polisi, Ofisi za Mitaa na Kata.

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya upatikanaji wa maji ni mbaya katika maeneo ya Msongola-Mpera, Msongola- Mvuti, Msongola-Mbondou, Msongola-Uwanja wa Nyani, Buyuni-Zavala, Buyuni, Buyuni-Kigezi, Zingiziwa-Nzasa, Chanika, Pugu Station, Kivule-Bombambili, Pugu, Ukonga, Gongolamboto na Msongola-Yangeyange. Naomba kujua kwa uhakika utekelezaji wa miradi ya maji Ukonga na Kata zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.