Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Bahati Ali Abeid

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. BAHATI ALI ABEID: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na miradi ya umwagiliaji; maeneo mengi ya nchi yetu haijamalizika na miradi mingi haikuwa kwenye kiwango chenye kuonesha kuwa hata ikimaliza haitanufaisha Watanzania na hasa ile miradi iliyosimamiwa na Kanda. Kanda hizi kwa asilimia kubwa, miradi waliyoisimamia haikumalizika, ilikuwa ni tatizo. Hivi ni kweli walikuwa ni wataalam waliosimamia miradi hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ni uhai kwa viumbe vyote. Ni vema Serikali tukipanga vipaumbele vyetu, ni lazima maji tuipe bajeti kubwa na siyo kuipunguzia bajeti. Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumzia kuongeza hiyo sh.50/= ili bajeti iongezeke. Hivi zile pesa za msaada wa India zimefikia wapi na hata kule Zanzibar?

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja