Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali iongeze tozo ya sh.50/= kwenye mafuta ili isaidie masuala ya maji, asilimia 70 iende vijijini na asilimia 30 mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, bili za maji ni kubwa sana hasa katika Mkoa wa Njombe na hasa katika Halmashauri ya Njombe Mjini. Naomba Serikali ifuatilie suala hili la bili lifungwe, maana wananchi wanalalamika sana kwa sababu ya bili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Njombe ni tajiri wa mito, lakini wananchi wanahangaika sana maji hayatoki; hata Njombe Mjini maji hayatoki, lakini watu wanaendelea kulipa bili kubwa. Maeneo ambayo maji hayatoki ni Mtaa wa Mpechi, Joshoni, Idunditanga, Sido, Ramadhani, Kibena na maeneo mengine. Naiomba Serikali iwasaidie wananchi hawa kwa kuwaboreshea miundombinu ya maji ili maji yaweze kutoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vingi vya Mkoa wa Njombe havina maji. Katika Wilaya ya Wanging’ombe kulikuwa na maji huko nyuma, lakini kwa sasa mabomba haya hayatoi maji, yameshaharibika; akinamama wanapata shida, wanakwenda umbali mrefu kutafuta maji. Naomba miradi hiyo ya maji ifike vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.