Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Mjini Kakonko ulitengewa fedha shilingi milioni 300 katika bajeti ya 2016/2017 na mradi ulishatangazwa na wazabuni kupatikana. Mradi haujaanza kwa sababu ya mikataba kutosainiwa. Nashauri kwamba mkataba usainiwe ili Mkandarasi aanze kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi mkubwa wa Mto Mgembezi – Kakonko ni mpya, unahitaji nguvu ya kifedha. Intake ilishajengwa, bado kuweka mabomba na tank (reserve). Mradi ukikamilika, utanufaisha Kata za Kusuga, Kakonko, Kanyonza, Kiziguzigu na Kasanda. Ushauri wangu ni kwamba Serikali iweke kipaumbele kwa maji haya ya mteremko (gravity water).

Mheshimiwa Naibu Spika, Miradi ya World Bank iliyopo Wilayani Kakonko yote imekwama kukamilika wakati fedha zilishatolewa. Miradi hiyo iko Vijiji vya Muhanga, Katanga, Kidudaye na Nyagwijima. Ushauri wangu ni kwamba Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri afike Kakonko kukagua miradi hiyo ili atoe ushauri wa nini kifanyike ili wananchi wanufaike na miradi hiyo.