Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Sanjo ina vijiji 24 na wananchi 120,000. Ina hali mbaya sana, haina hata bwawa wala mito, lakini imezungukwa na Ziwa Victoria. Maji yanatakiwa yatoke Lutale ambapo ndiyo chanzo, yaende Vijiji vya Kageye, Kayenze, Itandula, Langi, Makamba, Shilingwa, Kongolo, Chabula, Bugando, Nyashiwe, Ihayabuyaga, Welamasonga, Matale, Sese, Ihushi, Isangijo, Busekwa, Bujora, Kisesa, Kanyama, Wita, Welamasonga na Igekemaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Ndagalu ina vijiji 26 wakazi 86,000. Tarafa hii haina hata mto wala bwawa sasa wanafuata maji kilometa hadi 58. Tunaomba watu hawa muwaonee huruma, chanzo cha maji kitoke Nsola kwenda Misungwi, Kitongo, Lumeji, Nyang’hanga, Iseni, Mwamibanga, Buhumbi, Nyashoshi, Ng’haya, Mwabulenga, Nkungulu, Kayenze ‘B’, Chandulu, Bugatu, Salama, Kabila, Ng’wamagoli, Jinjimili, Nhobola, Kabale, Nyasato, Mahaha, Shishani, Isolo, Igombe, Ndagalu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa hii ya Ndagalu hata visima virefu havipo. Naomba tusaidiwe hata kwa dharura visima virefu kila kijiji pamoja na bwawa la Kabila likarabatiwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Naibu Katibu Mkuu, Engineer Kalobelo alifika akaona shida iliyopo akatuma wataalam kutoka MWAUWASA walifanya ziara wakaandika andiko la miradi hii miwili na Mkurugenzi alileta kwenye bajeti, Baraza likapitisha na tukapeleka hata Wizara ya Maji kwa Mkurugenzi wa Maji Bwana Mafuru, pamoja na kwa Naibu Katibu Mkuu Engineer Kalobelo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasikitika kutoona miradi hii kwenye bajeti. Jamani wanionee huruma hata waniwekee fedha za kuanzia ili kila mwaka waendelee kuniwekea, hususan naamini tutaongeza sh.50/= kwa kila lita ya mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukinisaidia hii, utakuwa umeokoa maisha ya Watanzania wengi sana wa Jimbo la Magu.

Mhshimiwa Naibu Spika, natanguliza shukurani.