Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Wizara hii kufanya kazi kubwa, naomba nichangie kidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kilolo haina tatizo la maji, bali ina tatizo kubwa la usambazaji wa maji. Wilaya ina Tarafa tatu; Kilolo: tatizo lipo Kata za Udekwa, Ukwega, Ng’uluwe na Idete. Mazombe: tatizo kubwa liko Ilula na Irole tatizo ni kubwa. Mahenge: hawa wanategemea sana kilimo cha umwagiliaji hivyo naomba Mheshimiwa Waziri atume timu toka Wizarani kwenda kuangalia tatizo kubwa ambalo lipo kwenye eneo hili. Mfano, Kata ya Mahenge kuna mabwawa ya umwagiliaji lakini changamoto ni idadi ya watu kwamba imeongezeka lakini intake zipo vile vile. Hivyo, ni bora timu yako ipite huko hasa katika vijiji vya Ilindi na Magana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Nyanzwa, hapa pia changamoto ni ongezeko la watu. Sasa bwawa leo linahitaji kupanuliwa na ahadi za viongozi, kama aliyekuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Pinda alitoa ahadi ya kuboresha bwawa hilo. Eneo hili pia hawana kabisa maji salama na safi ya kunywa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Ruaha Mbuyuni, pamoja na tatizo la udogo wa mabwawa lakini pia kuna matanki ya maji yamejengwa, lakini fedha za kuyasambaza maji hayo hakuna. Ombi langu kubwa ni kuomba Wizara hii itume timu kwenda katika eneo hili na kubaini malalamiko haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wetu alitoa ahadi ya kumaliza tatizo la maji Ilula, wakati wa kampeni. Sasa Mheshimiwa Rais anatarajia kwenda kuwashukuru wananchi hao, sasa wananchi lazima watampokea Mheshimiwa Rais kwa mabango, kwani bado tatizo lipo.