Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniheshimu, na mimi nakuheshimu sana na huwa sikosi nafasi ukikaa hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuwapa pole wale wenzetu wote waliofiwa kwa ajali ya gari kule Arusha, na mimi kwenye jimbo langu tulikuwa kati ya watu ambao tuliathirika kwa kufiwa na mtoto wetu kwenye kijiji cha Irambo. Kwa hiyo, poleni sana Watanzania wote na tunategemea haya mambo hayatajirudia tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuwapongeza hawa Waheshimiwa Mawaziri na Wizara nzima, ni watu ambao kwa kweli Wabunge watakubaliana na mimi, ukiongea nao hatakukatalia kitu, wana moyo wa kusaidia sana, hata ukienda Wizarani watakupokea vizuri sana. Hata hivyo, labda kitu kimoja tu, ukiwa na moyo inabidi vilevile uwe na maini. Nafikiri hapa leo tunazungumzia ni namna gani hawa tuwasaidie kwa moyo wao ule vilevile wamepewe na maini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya maji ni muhimu sana kwa Tanzania, lakini mimi nakubaliana na wenzangu wote kwamba hii bajeti iongezeke. Tozo ya kuongeza ya shilingi 50 ni muhimu na tusipinge hapa, kuna wengine wanafikiri ukiongeza hiyo labda itaongeza inflation, hapana. Mafuta tunanunua kwa dola, 2015 dola ilikuwa 2150, leo ni 2200, hata tukiongeza hiyo shilingi 50 haina impact yoyote kwenye inflation; na ukiongeza hiyo shilingi 50; na kwa ripoti ya EWURA tuliingiza mafuta kwa ajili ya matumizi ya Tanzania kama shilingi bilioni 3.4, ina maana tunaweza kuongeza kwenye bajeti zaidi ya shilingi 170,000,000,000, ni hela nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ninachoomba mimi hapa, kwa sababu kuongeza mapato ni suala lingine, je, haya mapato unakwenda kuongezea kwenye kikapu gani? Unaweza kwenda kuongeza kwenye kikapu ambacho kimetoboka, na hilo ndilo tatizo tulilonalo. Kwa sababu Sekta ya Maji kwa experience niliyonayo kwenye jimbo langu haina control kabisa, hela zote zinazopelekwa hazifanyi kazi ile inayotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mwaka 2010 Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya ilipewa zaidi ya shilingi bilioni
6.2 lakini leo hii ninapozungumza katika miaka yote hiyo hakuna mradi hata mmoja ambao unafanya kazi kwa hizo pesa zilizokwenda. Sasa tunaweza kuzungumzia hapa kuongeza pesa, unaongeza maji kwenye kikapu ambacho kimetoboka, unafanya kazi ya bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi ninachoomba hapa yawepo mambo mawili, iongezwe pesa kwenye bajeti kusaidia maji lakini vilevile kuwe na udhibiti wa pesa za maji. Udhibiti huo utasaidiwa kwa kuunda kile chombo cha Wakala wa Maji Vijijini na hiyo utekelezaji wake uje mara moja. Nalisema hilo kwa uchungu mkubwa kwa sababu Wabunge hapa ni mashahidi, niliuliza swali kuhusu matatizo, changamoto ya maji Mbalizi nikajibiwa kuwa hakuna matatizo ya maji Mbalizi na maji yapo ya ziada na wananchi mpaka leo wanashangaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo miradi ambayo sisi tulipewa, yote, ukiangalia orodha ya Wizara inaoneshwa hiyo miradi imekamilika. Sasa unauliza, huyu ni nani anayemdanganya Mheshimiwa Waziri? Ukionesha miradi imekamilika wananchi nao kule wanajua kuwa miradi imekamilika…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, ahsante.