Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza kabisa, niseme tu kwamba maoni mengi yaliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge na kwa sababu Wizara ya TAMISEMI inafanya kazi kwa karibu na Wizara hii ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, tutashirikiana kuhakikisha kwamba yale yote yanayohusu TAMISEMI tunayashughulikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili eneo ambalo limeguswa sana ni tozo na ushuru kwenye Mamalaka za Serikali za Mitaa kupitia Sheria ya Fedha, Sura Na.290 ambayo imebainisha vyanzo mbalimbali ambavyo vinatoka kwenye kilimo na vingine kwenye biashara, lakini hapa nitazungumza kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema ukweli ni kweli kabisa na Mheshimiwa Rais amesisitiza sana kwamba tufanyie kazi eneo hili la kodi kwa maana ya ushuru na tozo mbalimbali kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuhakikisha kwamba haziendi kutozwa kwa watu maskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya majukumu makubwa ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa ni kuhakikisha kwamba tunajenga uwezo na kujenga mazingira ya wananchi wetu ili kuweza kujitegemea na kuishi maisha bora. Watu hawa wanapojitegemea hivyo, kazi ya Serikali ni kujenga mazingira wezeshi, kuwafanya watu hawa waweze kumiliki lakini pia kuendesha biashara zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumegundua mambo yafuatayo katika utafiti na ndiyo maana baadaye nitasema nini tunafanya, kwamba kuna problem ya double taxation yaani kodi zinatolewa mara mbili katika jambo moja. Pia kuna kodi kufanana, kwa mfano, mahali ambapo unatozwa service levy haupaswi tena kutozwa produce cess, kwa hiyo, hizi unakuta kule zinakuwa zinatozwa zote kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumegundua kwamba kuna tozo hutozwa kwenye mitaji yaani tozo inatozwa kwa kupiga hesabu ya mtaji badala ya faida. Pia kuna tozo za ushuru usiozingatia mazingira ya uzalishaji, haya yote tumeyafanyia kazi na AG ataleta hapa mabadiliko ya sheria ambayo sisi kwa upande wa TAMISEMI tumeshamaliza tumepitia sheria zote, tumeangalia zile tozo zote, tunadhani nyingine zinahitaji kuletwa hapa ili tubadilishe sheria zilizopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tulitunga hapa sheria ambayo inatoza service levy hata kwa non corporate entity, yaani mtu ana kibiashara cha saloon unamtoza service levy 0.3% ya turn over, huu ni unyonyaji, haiwezekani! Hii ilikuwa inatozwa kwa corporate entity tu, kampuni kubwa ndiyo inatozwa lakini sio mtu ana saloon ya mtaji wa shilingi milioni tano unamtoza service levy, hii siyo sawasawa. Kwa hiyo, marekebisho hayo yote tutayazingatia na maandalizi ya sheria yako tayari, tutaleta hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.