Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kwa muda mfupi uliopo napenda niongelee suala la vinyungu ambalo limezungumziwa sana na Waheshimiwa Wabunge hapa ndani lakini vilevile wakati tunazungumzia hotuba ya Maji na Umwagiliaji nilitolea ufafanuzi jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba, suala hili ni la kisheria ambapo linalindwa na Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 pamoja na Sheria ya Matumizi Bora ya Ardhi ya mwaka 2007, vyote hivi ni katika kulinda vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema kwa Waheshimiwa Wabunge ni kwamba sisi kama Serikali hatujazuia vinyungu nje ya mita 60 lakini kama nilivyosema kwamba tutakwenda kuyaona maeneo hayo ambayo Waheshimiwa Wabunge wameyazungumza ili tuone yameguswa vipi na tuone hatua za kuchukua. Kwa hiyo, ahadi itabaki ile ile ya kwenda kuyaona maeneo hayo ya Waheshimiwa Wabunge ambayo wameyalalamikia na Serikali itachukua hatua katika jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala limezungumzwa dhidi ya Taasisi za Muungano yaani za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutokushirikiana katika kufanya utafiti. Nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba Taasisi zetu za Muungano na zisizokuwa za Muungano zinashirikiana vizuri sana hasa katika hili suala la utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Benki Kuu imefanya utafiti mwingi sana Zanzibar, zaidi ya tafiti 13 katika mazao mbalimbali mazao ya mpunga, mchele, minazi, karafuu na ripoti yake kukabidhiwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na inayafanyia kazi na inanufaika vizuri sana na tafiti hizi ambazo zinafanywa na Benki Kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, COSTECH ndiyo mratibu mkubwa wa tafiti za kisayansi pamoja na hizi za kilimo na imekuwa ikitoa fedha katika Taasisi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na zile za Zanzibar kwa mfano SUZA pamoja na IMS kwa maana ya Institute of Marine Science na tafiti zake zimekuwa zikileta tija kubwa sana. COSTECH wameweza kutoa zaidi ya bilioni tatu kwa ajili ya ku-facilitate tafiti nyingi ambazo zimefanyika Zanzibar na zimeleta tija kubwa sana katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.