Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yale yote niliyoyochangia pale uliponipa nafasi zipo baadhi ya changamoto za uvuvi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za kodi za samaki na dagaa mipakani ni kubwa sana, naiomba Serikali kuliangalia hili suala kwa ukaribu ili kunusuru gharama kubwa zinazoelekezwa kwa mvuvi. Lipo suala la Sheria ya Uvuvi ya mwaka 1973 ambayo ilitungwa kabla hata samaki aina ya sangara hawajapandikizwa katika Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba sheria hii aiendani na uvuvi wa kisasa, pamoja na yote nyavu hizi za inchi saba bado hazikidhi mahitaji ya uvuvi katika kina kirefu ambapo zimekuwa zikichukuliwa na mawimbi mazito pamoja na makundi ya samaki aina ya sangara. Hii ni kwa sababu nyavu hizo zinakua nyepesi. Hivyo basi, naiomba Serikali kutumia wataalam wake kuweza kutatua tatizo hili ili malalamiko haya yafike mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.