Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, mabadiliko ya vyeo yasiyoendana na mabadiliko ya mishahara. Kwa mfano, waliokuwa Nursing Officers waliambiwa kuwa ili waendelee kuwa na vyeo hivyo basi wanatakiwa kuwa na degree, lakini hata baada ya kwenda shule na kuwa na kiwango hicho cha elimu bado mishahara yao imebaki vile vile.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ni mafao ya kustaafu kwa Watumishi waliohamishwa kutoka Serikali Kuu (RDD) na kupelekwa Halmshauri (W). Mfano, Marcela Ndagabwene aliajiriwa 1986 hadi 1992 (RDD), 1993 hadi 2011 (DED). lakini baada ya kustaafu mwaka 2011 amelipwa sh. 1,915,311.20. Pia Ndugu Florida Mhate ameajiriwa mwaka 1979 na kustaafu mwaka 2010 na amelipwa sh. 1,445,569,28
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba msaada wako kwani aina ya Watumishi hawa ni wengi.