Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Naibu Waziri na Katibu Mkuu pamoja na Watendaji wote wa Wizara kwa kuandaa hotuba hii. Kwa kuwa nilichangia kwa kuongea kuna baadhi ya masuala ambayo sikuweza kuongea kutokana na muda. Naomba kuyachangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na NGO nyingi zinazofanya kazi zinazofanana katika eneo moja, hii huwachanganya wakulima kutokana na duplication ya kazi. Aidha, kuna baadhi ya wakulima wanaamini NGO zipo kwa ajili ya kufuja fedha. Mfano, kuna NGO zinafanya kazi eneo la Iringa Vijijini, ni budi Serikali ikawapa ushauri NGO’s wafanye mipango kwanza ili kujua NGO ipi inafanya kazi katika eneo lipi? Aidha, NGOs zinapoenda kuomba kibali cha kufanya kazi ni budi Halmashauri wakatoa ushauri, yale maeneo yaliyofikiwa na NGO yasipelekewe huduma na NGO hizo badala yake wawape maeneo mapya katika kutekeleza miradi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Extension Officers wapo wachache, hawana msemaji wa fani, kwani wakipelekwa katika maeneo ya Vijiji/Ward/Wilaya hawapati mafunzo ya mara kwa mara yanayoendana na teknolojia ya kisasa. Aidha, ukosefu wa vitendea kazi ni kikwazo kikubwa katika utekelezaji majukumu ya Mabibi Shamba na Mabwana Shamba. Vifaa mfano magari, pikipiki na ukosefu wa mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wadudu waharibifu hasa katika Kanda ya Kati, ndege waharibifu aina ya Kwelea Kwelea. Nashauri Serikali ifanye utaratibu wa kununua ndege yake ya kunyunyuzia dawa ili pindi inapotokea ndege waharibifu dawa ziweze kunyunyiziwa kwa muda sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Idara ya Mifugo ukurasa wa 106 wa hotuba umebainisha kupungua kwa uzalishaji wa maziwa. Nashauri Serikali ibaini maeneo na kugawa mashamba kwa wafugaji na wapate utaalam wa kupanda majani kwa ajili ya chakula cha mifugo. Aidha, ni budi Serikali ikapata idadi kamili ya wananchi ambao ni wafugaji wadogo wadogo nchini ili kubaini nao wanazalisha maziwa kiasi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado suala la unywaji maziwa shuleni upo katika kiwango kidogo, ni budi wadau mbalimbali wakashirikishwa ili waweze kusaidia suala la utoaji maziwa kwa watoto shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.