Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kwa maandishi Wizara hii muhimu kwa mustakabali wa uchumi wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu importation ya mbegu za kilimo, kwa nini tunaendelea kuruhusu makampuni makubwa kama Panner SIDCO ambayo hurb zao zipo nje ziendelee kushika kasi katika soko la mbegu? Serikali lazima ifikirie kuwezesha makampuni ya ndani na wakulima wetu kupitia Vyuo vya Utafiti kama Ilonga, ASA, kuwasadia wakulima kuzalisha mbegu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhakika wa chakula unaenda sambamba na uhakika wa mbegu. Lazima Taifa lijitafakari na kutenga bajeti ya kudumu kuwezesha makampuni ya ndani kuyajengea uwezo wa kutengeneza mbegu hasa zinazoendana na hali ya hewa ya mazingira tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako malalamiko ya wananchi juu ya mfumo wa NFRA na hii inatokana na urasimu wa Viongozi wa Vyama vya Ushirika ambao wanatumia mfumo huu kuwapa fursa wafanyabiashara wa mazao kuuza mazao badala ya wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba Maafisa Kilimo katika ngazi za Kata watumike kusaidia kuwatambua wakulima na kuwawezesha kupata fursa badala ya sasa hivi ilivyo kwa mfumo huu kwa nje unaonekana kuwasaidia wakulima, lakini wengine wanaumizwa na urasimu huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mbegu feki masokoni; mamlaka zinazohusika kwa nini zinashindwa kufanya kazi? Wakulima wananunua mbegu madukani hawana utalaam wa mbegu, lakini hakuna hatua za dhati za kuwakamata, kukagua maduka ya pembejeo za kilimo
na mifugo ili kubaini mbegu feki na mbegu zilizoisha muda wake wa matumizi. Mfano, viuatilifu holela vinavyoingia madukani kwa njia ya panya, mfano Mkoani Mbeya na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya wakulima na wafugaji katika mikoa mbalimbali ikiwemo Mkoa wa Morogoro katika Wilaya ya Kilosa, Mvomero, Kilombero na Wilaya ya Morogoro Vijijini. Serikali, Wizara ya Ardhi isaidie kufuta mashamba pori yasiyoendelezwa kwa miaka mingi. Mfano, Mvomero na Kilosa, Serikali ichukue hatua kubadilisha matumizi ya mashamba hayo. Mfano, NAFCO Kilosa yagawiwe kwa wakulima na wafugaji ambao migogoro yao inatokana na uhaba wa maeneo ya kilimo na ufugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mlundikano wa kodi au ushuru wa mazao kwa wakulima mfano, soko la mazao Kibaigwa. Ni kilio cha wakulima wengi wa Mikoa ya jirani na Morogoro; Kiteto na Dodoma ambao wanashindwa kupeleka mazao yao kutokana na ushuru wa mazao wa kila kituo cha kizuizi cha ushuru wa mazao. Ushuru huu ukiondolewa, utawasaidia wakulima kuacha kuuza mazao yakiwa mashambani na badala yake ushuru huu watozwe wafanyabiashara. Vinginevyo, wakulima wataendelea kuuza mazao yakiwa shambani na kwa lumbesa.