Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo, mifugo na uvuvi ni sekta muhimu sana kwa uchumi na maendeleo ya nchi na Watanzania kiujumla. Sekta hizi zimeendelea kutoa mchango mkubwa ikiwemo kuwa chanzo cha kipato kwa asilimia 65 ya Watanzania, kuhakikisha usalama wa chakula, kuchangia Pato la Taifa kwa zaidi ya asilimia 28 na mauzo ya nje kwa zaidi ya asilimia
24. Ingawa sekta hizi ni muhimu sana lakini zina changamoto nyingi sana ambazo zinaathiri ukuaji wake; changamoto hizo ni kama zifuatazo:-

(i) Utengaji na utoaji mdogo wa fedha za bajeti ya maendeleo.

(ii) Wataalam wa utafiti kuwa wachache ama kukosekana.

(iii) Miundombinu duni kwa mfano utoaji wa taarifa za tahadhari na upungufu wa viwanda vya bidhaa zake.

(iv) Athari za mabadiliko ya tabianchi, kwa mfano kuongezeka kwa ukame, magonjwa ya mimea na mifugo, mvua zisizotabirika na mashamba kuingiliwa na maji ya chumvi na kuathiri mazao na vyanzo vya maji baridi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwenendo wa bajeti ya Wizara hii kwa mwaka 2017/2018 si wakuridhisha japo kwamba sekta hizi hutoa mchango mkubwa sana kwa Taifa. Takwimu zinaonesha kwamaba wastani wa bajeti ya Wizara kwa sekta hizo ni asilimia 2.2 kwa kipindi hicho tu ya Bajeti ya Taifa ambacho ni kiwango kidogo sana ukilinganisha na lengo la kufikia asilimia 10 kama Serikali ilivyoridhia katika Azimo la Malabo kwa kipindi cha mikaka mitano ya mwanzo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo yangu kwa Wizara hii ni kuwa haijapewa kipaumbele cha kuridhisha katika Bajeti ya Serikali japokuwa vimeendelea kutoa mchango mkubwa kwa Taifa ukizingatia kwamba tunakwenda kwa kasi ya Tanzania ya viwanda. Pia mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuathiri maendeleo ya sekta hizi na Taifa, jambo ambalo pia limesisitizwa na Waziri wa Fedha na Mipando kwenye Bunge mwezi Machi 2017; kwa hiyo napendekeza yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba kuwe na utengenezaji wa bajeti halisi na utoaji wa fedha za kutosha na kwa wakati kwa kuwa wastani wa utoaji wa fedha kwa sekta hizi ni chini ya asilimia 60. Hivyo naishauri Serikali ifanye marejeo katika utaratibu wa utengaji wa fedha za bajeti ili kufuata uhalisia wa makusanyo yake japo kwa Mheshimiwa Rais ameonesha jitihada kubwa ya kupunguza rushwa na matumizi yasiyo ya lazima na tija kwa raia lakini utoaji wa fedha wa bajeti uwe wa kutosha na kwa wakati, kwa hiyo, Serikali inahitajika.

Mheshimiwa Mwenyeki, pia kuongeza jitihada na kuweka mikakati mahususi na kabambe ya upataji wa mapato ya nje ya vyanzo vya kodi. Taarifa ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kwa Bunge Machi mwaka huu inaonesha kuwa vyanzo vingine vya mapato kutofanya vizuri ukilinganisha na vyanzo vya kodi. Hii inajumuisha misaada ya wahisani, mapato ya Serikali za Mitaa na mauzo ya nje, pia uwekezaji mzuri wa misaada ya wahisani na mikopo tunayopata ili kupunguza na kuacha kabisa uteegemezi huo kwa kipindi kijacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuongeza utengaji wa bajeti ya maendeleo kutoka vyanzo vya ndani kwa mwaka 2016/ 2017. Vyanzo vya ndani vilichangia kwa asilimia 26 tu ya Bajeti ya Wizara ambapo mwaka 2017/2018 inategemewa kupanda mpaka kufikia asilimia 40 ya makusanyo ya mapato kwa vyanzo vya ndani kutokana na sekta husika kuboreshwa na kuwa za kisasa zaidi. Hii inajumuisha matumizi ya pembejeo na zana bora za kilimo, kuwekeza katika miundombinu bora ya kilimo, mifugo na uvuvi na kuboresha tafiti. Haya yakifanyika yatasaidia kufikia na kuvuka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli kwa Wizara ambayo bado yapo chini kwa mwaka 2016/2017 ambapo lengo lilikuwa ni kukusanya kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni nne kiwango ambacho ni kidogo sana ukilinganisha na uwezo wa sekta hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabadiliko ya tabianchi kupewa kipaumbele, yaani ni kuhuisha masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika bajeti ya Wizara na sekretalieti za mitaa. Ninatambua jitihada zilizofanywa na Wizara hii kuhuisha masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika mipango yao, hata hivyo bado hicho hakijafanyika vizuri katika bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ukizingatia masuala ya kijinsia, yaani ni kuandaa na kutoa taarifa za kibajeti zenye mchanganyiko na mchanganuo wa kijinsia. Taarifa hizi za mchanganuo zitasaidia zaidi katika mipango na maamuzi katika sekta hizo ambazo zinachangiwa zaidi na wanawake. Hivyo basi mahitaji maalum yatatambuliwa na kuwekewa mikakati mizuri na imara ya utekelezaji. Vilevile kuboresha mkakati wa kuwasaidia wakulima wanawake wadogo wadogo. Hivyo Wizara na Serikali kiujumla inahitaji kupitia upya na kuboresha utekelezaji wa kuwasaidia wakulima wanawake na wakulima wadogo wadogo ili waje na mrengo wa kijinsia na hivyo kuwasaidia ikiwemo katika upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuajiri Maafiasa Ugani wa kutosha, hii itaongeza uwezo wa Serikali kutoa elimu ya ugavi kwa sekta hizo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi. Hivyo agizo la kusitisha ajira zikiwemo za maafisa ugani lisitishwe, Wizara iombe kibali mara moja cha kutoa ajira kwa mamlaka husika, na pia suala hili liwekwe katika bajeti za Halmashauri zote zenye uhitaji ili kufanikisha utekelezaji wake. Pia kuboresha uwezo wa maafisa waliopo ili kuendana na mabadiliko ya taaluma na teknolojia kwa kupewa mafunzo rasmi ya vyuoni, semina elekezi na pia ziara ya mafunzo kwa maeneo mengine ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ya viwanda haitakuwepo kama kilimo hakitapewa kipaumbele na kuzitumia sekta hizi vizuri na kuziboresha na kuziwekea bajeti ya kutosha na kufika kwa wakati kwa maslahi ya umma na Taifa hili kwa ujumla wake. Vilevile kuweza kuithamini kauli yetu ya kuwa kilimo ni uti wa mgongo na kilimo kwanza yenye Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.