Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Tumbi kimesahaulika kwa ukarabati wa majengo, upungufu wa wakufunzi, mashamba darasa kutengewa fedha za kutosha. Mashamba darasa hayo yanatumika kwa kufundishia kwa vitendo; madai ya watumishi yalipwe kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu zao la tumbaku, natoa pongezi kwa kutatua tatizo la wakulima wa zao hilo kutoka Chama Kikuu cha Ushirika cha WETCU. Niombe Serikali kuhakikisha madai ya wakulima ambao walipunjwa na wanunuzi ili walipwe haki zao. Pembejeo zipelekwe kwa wakati, watumishi wanaodai haki zao WETCU walipwe kwani ni ya muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Benki ya Kilimo, nashauri benki hiyo tufunguliwe dirisha Tabora ili wakulima waweze kukopeshwa. Wakulima wakopeshwe matrekta ili wapunguze umaskini kwa kulima kilimo cha kisasa. Wakulima watafutiwe masoko ya uhakika kwa mazao yao. Tuombe benki iweze kusaidia wakulima wadogo wadogo hasa wanawake, wafugaji pamoja na wavuna asali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kupunguza zaidi idadi za tozo hususani kwenye zao la tumbaku ili bei ya uuzaji ipande. Kiongozi wa Ushirika angalau awe kidato cha nne, kwani kukosa elimu kwa viongozi kunachangia kuibiwa kwa fedha za wakulima. Pia mizani ya kupimia tumbaku (uzito wa kilo) iwe inakaguliwa mara kwa mara, masoko ya tumbaku yasicheleweshwe kwani kuchelewa kununua kunapunguza uzito, ndio ujanja wa wanunuzi na mawakala wao. Tuwasaidie wakulima wetu kama azma ya Serikali ya Awamu ya Tano.