Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hongera sana kwake Mheshimiwa Waziri Charles Tizeba na Naibu Waziri Mheshimiwa William Olenasha kwa kazi nzuri wanayoifanya pamoja na timu yao, Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara. Hotuba yao ni nzuri na imejitosheleza kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji lishe bora kwa wananchi wote wa Tanzania. Ni muhimu tuwahakikishie upatikanaji wa mboga na matunda kwa mwaka mzima kwa bei nafuu. Wizara ianzishe Drip Irrigation kila Wilaya kwa kutumia visima virefu. Kilimo hiki pamoja na kuboresha lishe ya jamii kitasadia kuongeza kipato hasa kwa makundi ya wanawake na vijana. Pia kitaongeza ukuaji wa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri zitembelewe na ukaguzi ufanyike kuhusiana na tozo kubwa wanazotozwa wavuvi. Yapo malalamiko ya kwamba wavuvi kule Mtwara wanalipa dola 500 kwa kila kilo moja ya samaki wanaovuliwa kutoka Msumbiji na hivyo kupelekea hasara kwani bei ya kuuzia huwa ni ya chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hongera sana kwa usimamizi mzuri wa zao la korosho. Kwa msimu huu umakini uongezeke katika ugawaji wa pembejeo kwa wakati na udhibiti wa kangomba. Kutokana na bei nzuri ya korosho ya mwaka uliopita wakulima wengi sasa wanaomba mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao mengine kama mbaazi. Wizara iangalie uwezekano wa kuanzisha mfumo huu kwa mazao mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na ninaitakia Wizara kila la heri.