Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Vinyungu na Mita 60 Kutoka kwenye Vyanzo vya Maji. Suala hili nalipeleka kwa Mheshimiwa Waziri kwa kuwa linagusa kilimo moja kwa moja japo usimamizi wa sheria ya mita 60 inasimamiwa na watu wa mazingira kupitia NEMC

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo cha vinyungu kwa lugha nyepesi tunaweza kusema ni kilimo cha mabondeni. Sasa tafsiri hii ya mita 60 kutoka vyanzo vya maji au kingo za mito ni tofauti sana na kilimo cha vinyungu. Vinyungu (Iringa na Njombe) au masebula (Kigoma, Katavi, Rukwa na Kagera) ni kilimo cha muda mrefu ambacho ni sawa na asilimia 50 ya maisha ya wananchi wanaoishi kwa kutegemea vinyungu miaka nenda miaka rudi na hakijawahi kuathiri mtiririko wa maji; na ndiyo maana mpaka leo ni mikoa hiyo pekee ambayo vyanzo vya maji vimeendelea kuwepo. Wananchi wanaheshimu vyanzo vya maji, wanatunza maji tena kwa njia ya asili; hivyo vinyungu si tatizo wala chanzo cha kuvuruga vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, athari; Mkoa ya Iringa, Mbeya, Njombe, na Ruvuma/Rukwa imeendelea kuwa kimbilio la chakula miaka yote kwa sababu pamoja na mashamba ya kawaida vinyungu vimekuwa na mchango wa zaidi ya asilimia 40 ya chakula katika mikoa hiyo kuanzia mahindi, viazi na mazao ya mbogamboga kwa hiyo kuibuka na kusema tunazuia kilimo cha vivyungu maana yake tunaandaa mazingira ya kuleta njaa kwenye maeneo hayo. Jambo hili litazamwe upya na maamuzi yanayohusu kilimo cha vivyungu, wananchi na sisi viongozi wao tushirikishwe ipasavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Suala la Mbolea. Ukweli ni kuwa mfumo wa ruzuku ulinufaisha watu at individual level wakiwemo wafanyabiashara na baadhi ya watendaji wa Serikali. Uamuzi wa kuagiza kwa mkupuo (bulk) utasaidia. Angalizo ni kama ifuatavyo:-

(a) Haitakuwa na maana ikiwa mbolea itachelewa kuwafikia wakulima wa mbolea vijijini. Kwa mfano kwetu Iringa msimu unaanza Oktoba kuandaa mashamba na kufikia Novemba tarehe 15 wanakuwa wameshapanda bila kujali mvua zipo au hazipo, mbegu hutangulia ardhini. Sasa katika hali hiyo ni vyema mbolea iwafikie mapema Oktoba

(b) Kuhusu upatikanaji, jambo hili ni kubwa sana na mtego kwa Serikali hasa kama upatikanaji na usambazaji utakuwa duni. Ushauri wangu, maandalizi kwa kila msimu yafanywe mapema Mheshimiwa Mwenyekiti, Wanasiasa VS Ushirika. Serikali imedhamiria sana kutusaidia kupitia ushirika na hasa SACCOS. Baadhi ya maeneo Halmashauri zimeshapokea fedha kwa ajili ya SACCOS za vijana na hata zile milioni 50 kwa kila kijiji, matarajio ni kuwa zitapitia ushirika na SACCOS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, pamoja na uwepo wa Sheria bado wanasiasa directly or indirectly wanajihusisha kwenye SACCOS na ushirika na wengine ni viongozi. Hili ni bomu mbele ya safari kwa sababu linaweza kuibua chuki, upendeleo na baadaye kuvuruga ushirika na SACCOS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri. Pamoja na uwepo wa sheria ni vizuri Wizara ikasimamia utekelezaji wa sheria na kupitia TAMISEMI mwongozo/waraka ukatolewa kuwaeleza Mamlaka za Mikoa (Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri) kuwa wanasiasa hawaruhusiwi kuwa sehemu ya ushirika/SACCOS ili kuepusha migongano na hatari ya kuvuruga ushirika/SACCOS, naomba kuwasilisha.