Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii muhimu ina changamoto nyingi sana ikilinganishwa na mikakati inayoendana na utatuaji wake. Hii ipo dhahiri kabisa ukiangalia umuhimu wake unaopewa na Serikali Kuu kupitia budget allocation na upatikanaji fedha husika kwa shughuli mbalimbali inayohusu sekta hii. Changamoto hizi zinajulikana ila hazipewi attention inayotakiwa kama:-

(i) Vitendea kazi/vifaa/teknolojia za kilimo, uvuvi na ufugaji asilimia kubwa ya wananchi hutumia vifaa kale kama majembe na mashoka katika century hii;

(ii) Tegemezi ya kilimo cha mvua;

(iii) Mfumo wa masoko ulio una upungufu mwingi na uliopitwa na wakati. Mfano, hatuna ama hakuna reliable, efficient market data na information;

(iv) Maeneo mengi hakuna kabisa/ipo katika hali hafifu ya adequate production and post-harvest technologies;

(v) Pembejeo za kilimo; utengenezaji, upatikanaji na usambazaji wa mbolea, mbegu ni hafifu na hauzingatii microclimate ya maeneo husika, ucheleweshwaji, low quality;

(vi) Extension officers; kuna upungufu mkubwa. Hawa ni kiungo muhimu katika kusaidia wakulima, wavuvi na wafugaji kwa ajili ya kuelimisha na consultation kuipa umuhimu kupitia budget, research, Maafisa Ugani kutahakikisha kupatikana kwa chakula (food security) katika nchi yetu;

(vii) Kuimarisha Taasisi za Utafiti mfano, TAFIRI na TAWIRI. Bila kuwa na takwimu siyo rahisi kufanya maamuzi. Taasisi hizi inabidi kupewa kipaumbele kwa kuhakikisha zinatengewa bajeti mahsusi kwa ajili ya tafiti, kukusanya data na kuajiri watafiti;

(viii) Sekta ya uvuvi; Serikali iangalie sekta hii kwa jicho la pekee ni eneo lenye potential kubwa sana katika kuimarisha uchumi wa wananchi na nchi kwa ujumla wake. Sekta inahitaji kuimarisha research and data collection, kuwa na bandari ya uvuvi, kudhibiti uvuvi haramu, kuimarisha Deep Sea Fishing Authority (monitoring, licensing e.t.c);

(ix) Wizara inahitaji kuwa strengthened kupitia budget allocation/ release of funds ili iweze kusimamia sera yake. Kiwango cha bajeti inayokuwa allocated inaenda kinyume na maazimio ya Malabo. Kwa kipindi cha takribani miaka 10 Serikali imekuwa ikitenga chini ya asilimia mbili ya bajeti ya Taifa. Hata fedha hizi zinazotengwa kwa asilimia kubwa zimekuwa zikitolewa chini ya asilimia 50.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muktadha huu ni dhahiri Tanzania haitakaa ibadilike katika kukuza uchumi wake. Wizara inatakiwa kuja na mipango mikakati katika kuhakikisha sekta hizi muhimu (kilimo, mifugo na uvuvi) zinatuvusha kutoka katika umasikini.