Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kupunguza kodi mbalimbali na kuanzisha utaratibu wa bulk procurement ili kupunguza bei za pembejeo na hasa mbolea, lakini tunaomba isije ikatokea kama mwaka jana bei zilitangazwa lakini ikawa hakuna utekelezaji wowote. Mfumo wa vocha unakiua chama na Serikali mambo yafuatayo ni muhimu kupewa uzito unaostahili:-

(i) Kukuza kilimo; naamini kuwa kilimo kilichopo kwa sasa ni kilimo kidogo cha kupata chakula tu, nchi haiwezi kuendelea kwa kilimo hiki lazima yaanzishwe mashamba makubwa ya kibiashara ambayo yatatoa ajira rasmi kwa watu wengi, yatazalisha kwa tija na kutumia mbegu bora na zana za kisasa yaani commercial farming. Bila kufanya hivyo, tutaendelea kuimba bila mafanikio makubwa, hili linawezekana kama ilivyokuwa siku za nyuma.

(ii) Kufufua kilimo cha kahawa. Kwa miaka mingi zao la kahawa lilikuwa ni kitovu cha mazao ya biashara.

Hata hivyo, zao hili limeporomoka sana kiuzalishaji nchini. Lazima mkakati wa kulifufua zao hili uandaliwe haraka iwezekanavyo.

Sambamba na hilo, Chama cha Wadau wa Kahawa kiliunda TACRI kwa ajili ya kufanya utafiti wa zao la kahawa. Taasisi hii ilipewa majengo na maeneo yaliyokuwa chini ya Serikali. Hata hivyo, hivi sasa taasisi hii inakabiliwa na changamoto kadhaa. Hivyo, ili kuendeleza utafiti, napendekeza Serikali iichukue taasisi hii na kuifanya kama wakala wa Serikali ili kuongeza ufanisi na tija katika utafiti wa zao la kahawa. Zao hili ni muhimu sana kwa maendeleo ya uchumi wetu.

(iii) Suala la Benki ya Kilimo; Benki hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya kilimo. Ni vizuri kufungua matawi katika mikoa yenye kilimo sana ili kuwakopesha wakulima wengi, suala hili ni muhimu sana.