Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa namna inavyoendelea kufuta kodi, tozo, ushuru na ada ambazo zinaleta kero kwa wananchi hususan wafanyabiashara kama vile tozo ya afya ya kusafirisha mifugo nje ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ifute tozo ya kusafirisha mifugo nje ya Mkoa katika Minada ya Upili, kwa mfano, Mnada wa Mhunze, Wilaya ya Kishapu, Serikali Kuu hukusanya tozo zote, ushuru Sh.5,000/= kwa ng’ombe na tozo ya kusafirisha ng’ombe nje ya Mkoa Sh.2,500/= jumla Sh.7,500/
=, zote huchukuliwa na Serikali Kuu na Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu haipati kiasi chochote cha fedha. Naomba permit ya Sh.2,500/= iondolewe ili kumpunguzia mzigo mfanyabiashara wa mifugo ile Sh.5,000/= inatosha kabisa Mkoa kugawana na Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.